Kulwa Kikumba (Dude)
Jacqueline Wolper
Issa Mussa (Claude)
IMEKUWA ni kawaida katika tasnia ya filamu kuwasikia wasanii au watayarishaji wa filamu nchini kuulalamikia mfumo wa soko la filamu uliopo, hasa katika hili sakata linaloendelea hivi sasa kati ya wale walio chini ya Shirikisho la Filamu na Msambazaji mmoja mwenyewe nguvu anayelalamikiwa kuhodhi soko la filamu, ingawa ni haki yake kujipangia mfumo anaodhani utamsaidia kuuza kazi zake kwani hakuna mtu anayefanya biashara kwa ajili ya mtu mwingine.
Jina la kampuni na msambazaji anayelalamikiwa vimekuwa vikitajwa sana kila mara wanapokusanyika wasanii na watayarishaji wengi wa filamu nchini ambao wamekuwa wakiwatupia lawama wasambazaji hao wa kazi zao kwa madai kuwa,