Ukurasa wa facebook unaweza kutumika kutangaza sinema
Pia unaweza kutumia ukurasa katika mtandao wa Youtube
TASNIA ya filamu nchini ni
sawa na mtoto yatima lakini hali hii isiwe sababu ya kutufanya kulipua kazi
zetu, bali tunapaswa kuangalia namna iliyo nzuri itakayotuwezesha kuboresha
kazi zetu na kufanikiwa katika soko la ndani na hata nje ya Tanzania . Nimewahi kudokeza katika siku za nyuma kuhusu
vigezo muhimu viwili vinavyoweza kutuongoza katika dhana nzima ya mafanikio hasa
tunapolifikiria soko la filamu: Maudhui/Mahitaji ya Watazamaji na Jukwaa la
Uwasilishaji.
Tunapaswa kwanza kuwaelewa watazamaji
wetu kabla ya kufanya chochote, kwani ni hatua muhimu sana katika mchakato wa biashara ya filamu.