Jun 14, 2011

Tetesi: Ufuska na udharirishaji Bongo Movie Club

 Timu ya Bongo Movie Club ndani ya Mwanza

 Wasanii wa kike wa Bongo Movie Club

 Baadhi ya wadau wa Bongo Movie Club

Bongo Movie Club wanajiandaa kwenda Dodoma kwa ajili ya mechi yao na Wabunge hapo Ijumaa, lakini tayari kuna kashfa imeikumba club hiyo na viongozi wanajitahidi kuzima kashfa isijulikane kwenye vyombo vya habari kabla hawajacheza na wabunge.

Jana kutwa nzima na hata leo wana kikao cha kuweka mambo sawa hasa. Nimebahatika kuipata
meseji iliyotumwa na Msani mmoja wa kike kwenda kwa viongozi wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) akiwalalamikia, meseji yenyewe ni hii (sijaongeza neno ingawa majina ya wahusika nimeyahifadhi):

Ni msg yenu VIONGOZI kabla ya safari ya Dodoma; Kumekuwepo unyanyasaji mkubwa kwenye CLUB, ngono, majungu na ufisadi. msanii wa kike aitwaye (linatajwa jina) kagaragazwa sana na (jina la msanii wa kiume) walipokwenda Mwanza. (Jina la kiongozi mmoja wa club) kawagaragaza (linatajwa jina) na (linatajwa jina), na bado kuna wengine anawahitaji, tena kwa nguvu, nyie mmekaa kimya!


Huyo (msanii aliyemdharilisha mwenzake Mwanza) na (huyu alikuwa kiongozi wa TAFF enzi zile) wamegeuza CLUB sehemu ya kujipatia pesa kwa mapedeshee. ONYO hatukuja kugarazazwa tuheshimiwe la sivyo tutaripoti kwenye vyombo vya habari.

 
Mwisho wa kunukuu. Hapo kwenye maneno yenye RED nimebadili maneno yaliyoandikwa kwa sababu za kimaadili.
 
Inasikitisha sana kuona tabia kama hizi zikijitokeza kwa watu tunaoamini kuwa ni kioo cha jamii na waliopaswa kuwa mfano mzuri kwenye jamii yetu.

No comments: