Jan 5, 2011

BASATA yaja na siku ya Msanii

Kazi ya sanaa iliyopo Idara ya Sanaa ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam

 Katibu Mtendaji wa Basata, Ghonche Materego

BARAZA la Sanaa la Taifa (Basata) mwaka huu linatarajia kuandaa Tamasha kubwa la Wasaanii ambalo litakuwa likifanyika kila mwaka likiwa na jina la Siku ya Msanii wa Tanzania.

Katibu Mtendaji wa Basata, Ghonche Materego aliyasema hayo siku ya Jumatatu wiki hii alipokuwa akiwasilisha mada kwenye Jukwaa la Sanaa linalofanyika kwenye ukumbi wa Baraza hilo kila Jumatatu. Gonche alisema kuwa tamasha hilo ambalo litakuwa likipambwa na burudani kemkem kutoka kwa wasanii wa sanaa mbalimbali hapa nchini litakuwa ni maalum kwa ajili ya kuenzi sanaa kwa vitendo.

No comments: