Sep 25, 2013

Fursa muhimu kwa wasanii na wadau wa filamu



Jengo la Shule ya Biashara ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam


Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, UDSM, kimeandaa kozi ya uandishi wa filamu. Ni kozi ya siku kumi itakayoanza tarehe 1 mpaka 11 Oktoba. Kozi hii imetangazwa magazetini wiki iliyopita. Huu ni ujumbe utakaosaidia kufikisha ujumbe kuhusu fursa hii kwa wadau mbalimbali. Kozi hii itafanyika kwenye jengo la Shule Kuu ya Biashara (UDBS) ikilenga kuwezesha uandishi wa miswada ya filamu kwa kupitia ngazi zote kama vile sanaa ya uandishi wa miswada ya filamu, maandalizi kabla ya kuandika, kanuni za uandishi na usanifu wa mswada wa filamu, na muundo wa andiko la filamu.

Gharama za kozi hii ni Tsh. 300,000 (laki tatu). Gharama hizo ni kwa mafunzo, vifaa, chakula na Certificate ya UDSM.

Kujisajili au kwa taarifa zaidi mwombaji anaweza kuwasiliana kwa:
+255 754 288595 au +255 715 000366 au kaymollel@yahoo.com

No comments: