May 4, 2012

Zitto Kabwe, Halima Mdee na wasanii kibao ndani ya wimbo wa Sajuki


Sadik Juma Kilowoko Sajuki katika picha tofauti.
Kushoto alivyo sasa na kulia wakati akiwa mzima


Picha hizi zinawaonyesha Sajuki na mke wake
Wastara Juma katika hali ya furaha

Waheshimiwa wabunge wametoa track inayoenda kwa jina la "Nimepoteza Mboni Yangu" kwa ajili ya kuhamasisha kumchangia pesa za matibabu msanii Sadiki Juma Kilowoko maarufu kama Sajuki wimbo huu utaanza kusikika katika kituo cha Clouds FM.

Watu wamekuwa wakihamasishwa kuchangia kwa kutuma pesa kwenye Account No. 050000003047 AKIBA BANK, jina la mwenye account ni Wastara Juma ambaye ndiye mke wa Sajuki au watume pesa kupitia MPESA No. 0762189592.

Wimbo huu ni maalum kwa Sajuki ambae anahitaji mchango wa hali na mali kuokoa maisha yake. Sajuki anasumbuliwa na uvimbe tumboni na mwezi huu anahitajika kusafiri kwenda nchini India kwa matibabu. Wimbo huu unatoka katika filamu aliyowahi kuifanya na mkewe ya ‘MBONI YANGU.’

Na wimbo huu upo ndani ya filamu hiyo aliuimba Wastara. Umeurekodiwa tena kuhamasishana kuchangia na utaanza kusikika kesho katika kituo cha Clouds FM na video ya tukio zima la kurekodi itaonekana Clouds TV.

Kesho hiyo hiyo Clouds watahakikisha wanakusanya angalau Tsh milioni 12 na wanawaomba sana Watanzania wengine kushiriki katika hili.

Baadhi ya wasanii na waheshimiwa walioshiriki katika "Nimepoteza Mboni Yangu" ni pamoja na Wastara mwenyewe na Vick Kamata, Amini, Barnaba, Peter Msechu, Madee, Rachel, Wema Sepetu, Mzee Yusuph, Pro Jay, Afande Sele, Fid Q, Chid Benz, Linex, Queen Darlin, Shilole, Ali Kiba, William Mtitu, Ester Bulaya, MwanaFA, Halima Mdee, January Makamba ,Zitto Kabwe na Khadija.

Tahadhari.

JIHADHARI NA MATAPELI... unapotuma MPESA ili kutoa mchango wako wa SAJUKI hakikisha jina utakaloliona ni la mke wake ambae ni WASTARA JUMA. Kuna mtandao fulani aliokuwa anautumia mwanzo watu walihamisha salio kwa kuiswap namba yake…

No comments: