Dec 15, 2010

Changamoto yatolewa kwa wasanii kuthamini kazi zao

Vincent Kigosi (Ray)

Emmanuel Myamba maaruf kama Pastor Myamba
 Jalida la Baab Kubwa linalopamba 
kichwa cha habari kuhusu wasanii matajiri

Wasanii nchini wameshauriwa kuthamini na kuheshimu kazi zao za sanaa ili ziweze kuwakomboa kiuchumi na kutokuwa tegemezi. Kauli hii imetolewa na Ofisa Utamaduni wa jiji la Mwanza, Rosemary Makenke alipokuwa akiwasilisha mada iitwayo "Sanaa ni Ajira, Tuithamini" kwenye Kikao cha Nane cha Sekta ya Utamaduni kilichofanyika jijini Mwanza.

Ofia Utamaduni huyo alisema kuwa wasanii sharti wajiheshimu wao na kazi zao za sanaa wanazozifanya katika jamii kwa kuwa kazi ya sanaa kwa sasa ni ajira. Pia alisema kuwa sheria ya hakimiliki bado haisimamiwi kikamilifu na kwamba jasho na kazi za wasanii zinaendelea kuporwa na wajanja wachache kila siku.
katika kikao hicho pia kilihudhuriwa na wasanii maaruf, Jacob Stephen maaruf kama JB na Mrisho Mpoto "Mjomba" ambao walikuwa kivutio kwenye mkutano huo.

No comments: