Sep 21, 2010

Uzinduzi wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF)

 Umati wa watu waliohudhuria uzinduzi huo

Shirikisho la Filam Tanzania (TAFF) lilizinduliwa rasmi katika viwanja vya Leaders Club siku ya Jumamosi Septemba 18, 2010 na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, wasanii wa filamu na wadau mbalimbali.

Akifungua tamasha hilo Rais wa Shirikisho, Saimon Mwakifamba maaruf kama Jaspa alianza kwa kutoa shukurani kwa serikali kwa kulitambua Shirikisho la Filamu na kazi yao ya kwanza itakuwa ni kutetea maslahi ya wasanii na wadau wote katika tasnia ya filamu kwani mapato wanayopata ni kidogo sana na hayaendani na ugumu wa kazi husika. Vile vile Jaspa alisema kuwa wao kama TAFF wamedhamiria kuanzisha tamasha la filamu litakalojulikana kama Nyerere Film Festival na litaanza mwaka huu litakapofanyika kwa mara ya kwanza hapo Disemba.


No comments: