Mar 21, 2012

Jifunze kuandika Script ya Filamu kitaalam kwa kutumia Video

Tunamuenzi vipi Mzee Kipara?

. Alitumia sehemu kubwa ya maisha yake katika sanaa
. Aliishi maisha ya mateso makubwa mno kuliko jina lake
Mzee Kipara enzi za uhai wake akiwa kazini

Mzee Kipara wakati akiwa anaumwa 
    “Buriani Mzee Kipara”. Maneno yaliyoanza kusikika siku ya Jumatano ya Januari 11, 2012, baada ya saa 2:00 asubuhi, ambapo Mungu aliichukua roho yake na kumpumzisha na maumivu makali ya muda mrefu aliyokuwa akiyapata.

    Neno Buriani ni neno lililotawala kwenye machapisho mbalimbali zikiwemo wavuti (website), mitandao ya kijamii na blogu mbalimbali na lingeweza kumtoka binadamu yeyote aliyeshuhudia, kufuatilia ama kusoma kwa ukaribu sana kuhusu maisha ya mateso ya Mzee Kipara kabla ya umauti wake.

    Mar 2, 2012

    Sasa tujikite kutengeneza filamu fupi.

    * Zinalipa zaidi kuliko filamu ndefu
    Fasta Fasta, moja ya filamu fupi za Watanzania ambayo imefanya vizuri katika soko la kimataifa

    WIKI iliyopita katika ukumbi wa Baraza la Sanaa la Taifa (Basata), Chama cha Waongozaji wa Filamu Tanzania (Tafida) kiliandaa mafunzo maalum ya siku tatu kwa waongozaji wa filamu nchini, mafunzo yaliyotolewa na wataalam wawili kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Dodoma. Mafunzo haya yalifungwa na Bodi ya Ukaguzi wa Filamu na Michezo ya Kuigiza, ambao walipongeza sana juhudi hizi za Tafida kuyaandaa.

    Lengo kuu la mafunzo haya lilikuwa kujaribu kuongeza uelewa kwa waongozaji wa filamu ambao hawakubahatika kwenda shule za filamu kusomea.