Dec 23, 2015

Ni vema kufanya utafiti kabla hujawadharau Wasanii

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Moses Nnauye

WIKI iliyopita kwenye gazeti la Raia Mwema kulikuwa na makala yenye kichwa: “Baraza jipya la mawaziri, mkorogo usio hamasa kwa mabadiliko”, kutoka kwa mwandishi ninayemheshimu, Joseph Mihangwa. Nimekuwa msomaji mkubwa wa Mzee Mihangwa (kwangu ni sawa na baba’angu), kwa miaka mingi, nimekuwa msomaji wake na sijawahi kufikiria kumkosoa. Lakini nadhani ameteleza kidogo kwa kubeza juhudi za wasanii wa nchi hii.