Dec 28, 2016

Wasanii mmejipangaje kwa mwaka 2017?

· Ni wakati sasa mfikirie kuwa na dira

Wafanyuakazi wa Mamlaka ya Mapato (TRA) walipotembelea wauzaji wa filamu za Tanzania kuhakiki kazi zenye stempu za TRA

Mmoja wa wasanii wa filamu Tanzania, Vicent Kigosi, maarufu kama Ray

KWA Tanzania hakuna msanii yeyote anayeweza kusimama na kujisifu kwamba anakula halali kulingana na wingi wa jasho lake. Kila mmoja anatambua kuwa kuna mfumo kandamizi unaonyonya jasho la wasanii. Na ili kuendelea kuwanyonya, sasa wameaminishwa (na wale waliolishika soko) kuwa soko la kazi zao limekufa.

Wameaminishwa hivyo kwa kuwa soko la kazi zao linadhibitiwa na wafanyabiashara wachache, wasiozingatia taaluma na wasioongozwa na weledi. Ki ukweli kwa sasa soko halieleweki kabisa! Hali hii imesababisha watu kushindwa kutofautisha iwapo wanachokiona ni filamu, maigizo au mkanda wa harusi wenye “taito” za majina ya wasanii na wafanyabiashara wenye asili ya Kiasia!