Oct 21, 2015

WITO KWA WASANII: Kuna maisha hata baada ya uchaguzi

Baadhi ya wasanii wa Filamu wakiwa kwenye uzinduzi wa Kampeni za mgombea Urais wa Chadema anayeungwa mkono na UKAWA, Edward Lowassa
MWAKA HUU ninashuhudia mihemko ya ajabu ya kisiasa kwa wasanii kushabikia siasa na wanasiasa! Kwa mara nyingine tena nashuhudia namna wasanii wa fani mbalimbali wanavyodhihirisha umuhimu wao katika kipindi hiki cha uchaguzi mkuu, wakihusika katika kampeni za vyama, na kwa wagombea wa ngazi tofauti.

Nilipoona mihemko hii nilijiuliza kama kuna manufaa yoyote wanayopata kwa kushiriki kampeni hizi? Jibu likawa, yapo, kwani hiki ni kipindi cha mavuno kwa wasanii.

Je, unajua kuwa Filamu ya Yesu imerudiwa upya?

Muigizaji wa filamu ya Yesu, Brian Deacon

TAKRIBAN baada ya miaka 35 tokea sinema ya Yesu iliyoigizwa na Brian Deacon, muigizaji ambaye watu wengi wa kizazi cha siku hizi huamini kuwa ndiye Yesu, imerudiwa tena katika mfumo wa hali ya juu, kuanzia picha na hata uchanganyaji wa sauti.

Jesus, filamu ambayo ndiyo imevunja rekodi na inaongoza duniani kwa kutafsiriwa kwenda lugha nyingi, kwani kwa mujibu wa kitabu cha kumbukumbu cha Guiness, (Guiness World Record) filamu hiyo imetafsiriwa kwenda lugha 1,197 tofauti duniani kote, na kutazamwa na zaidi ya mara bilioni moja, huku watu zaidi ya milioni mbili wakiokoka kutokana na kutazama sinema hiyo.

Oct 7, 2015

KAMPENI 2015: U wapi uchumi na utajiri wa wasanii? - 2

Wasanii wa filamu, Anti Ezekiel na Jackline Wolper,
wakiunga mkono siasa za Chadema
Msanii wa vichekesho, Steven Mengere (Steve Nyerere),
katika mikutano ya CCM
WIKI HII nimelazimika kuendeleza mjadala wa ‘uchumi na utajiri wa wasanii’, hasa baada ya baadhi ya wasomaji wangu kunitumia ujumbe kutaka ufafanuzi katika mambo fulanifulani. Hata hivyo, wengi wao wanakubaliana na hoja yangu kwamba sanaa siyo sekta ya kuchezewachezewa, wala haipaswi kupuuzwa hata kidogo na wanasiasa wetu.

Sep 30, 2015

KAMPENI 2015: U wapi uchumi na utajiri wa wasanii?

Wasanii waliopo katika kampeni ya Mama Ongea na Mwanao mpigie kura Dk. Magufuli
KAMPENI za Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu zimepambwa zaidi na wasanii mbalimbali. Kumekuwepo na mhemuko wa ajabu wa wasanii kujitokeza kwenye majukwaa ya siasa, wengi wao wakijipambanua kuwa wafuasi au mashabiki wa vyama na wanasiasa fulani. Zikiwa zimesalia siku 22 tu kabla ya kupiga kura kuichagua serikali ijayo (Rais, Wabunge na Madiwani), hali bado ni ya mashaka kwa sekta ya sanaa.

Wasanii wanatumika kwa kiasi kikubwa kwenye majukwaa ya siasa, kiasi cha mikutano kugeuka kuwa matamasha ya burudani, huku wakiwa hawajui majaliwa yao kuhusu ustawi wa sekta ya sanaa, zaidi ya kupigwa porojo na ahadi zisizotekelezeka.

Sep 16, 2015

Sekta ya filamu Tanzania imekosa uhalisia


KATIKA wasanii mastaa ambao wangepaswa kuishi maisha mazuri hapa Tanzania, wasanii wa filamu ndiyo wangepaswa kuwa wanashikilia chati za juu kutokana na jinsi kazi zao zinavyotengeneza fedha nyingi. Kwa mujibu wa takwimu, kazi za wasanii hao zimekuwa zikiingiza fedha nyingi tofauti na ilivyokuwa awali, lakini maslahi hayo hutofautiana kwani wapo baadhi ambao hawashikiki.

Sep 9, 2015

Tuache utengenezaji sinema wa kulipuwa


SEKTA YA FILAMU nchini imekuwa inakua kwa kasi na kuwa kimbilio la vijana wengi, hata wale walioshindwa (failures) katika sekta zingine. Ukuaji wake umeambatana na changamoto nyingi katika kufikia ubora unaokubalika kimataifa kwenye filamu zetu.

Filamu ni nguzo muhimu sana ya Utamaduni wa nchi. Filamu zimeibuka kuanzia karne ya ishirini na baadaye kuwa kishawishi kikubwa na mawasiliano ghali katika karne ya ishirini na moja. Hakuna aina nyingine ya sanaa ambayo imesambaa kwa ufanisi na kuonekana kuvuka mipaka ya kiutamaduni katika mataifa mengi kama hii.

Aug 26, 2015

Je, tunaweka mipaka kwa watoto kutazama televisheni/filamu?

Watoto wanaangalia televisheni

MAJUZI jirani yangu mmoja (ambaye amenunua kisimbuzi hivi karibuni) aliniita nyumbani kwake na kuniomba nimsaidie kuweka namba za siri (password) kwenye baadhi ya chaneli za televisheni yake ili kuwadhibiti watoto wake wasiweze kuangalia sinema na vipindi visivyo na maadili. Aliamua kufanya hivyo baada ya kugundua uwepo wa chaneli zinazoonesha mambo yenye ukakasi.

Kwa sasa ni jambo la kawaida sana kwa watoto wengi kutazama filamu, televisheni, video, kucheza michezo (games) ya kompyuta, na kutumia Intaneti. Kulingana na makadirio fulani, watoto na vijana hutazama na kuvitumia vyombo vya habari kati ya mara 20 au 30 zaidi ya wakati wanaotumia kufanya mambo na familia zao. Jambo hilo huwafanya watoto wapate habari nyingi zenye kudhuru.