Jun 25, 2014

USHINDI WA SHOESHINE FESTICAB: Kwanini hatutilii maanani filamu fupi?

 Amil Shivji


TAKRIBAN wiki mbili zilizopita nilikuwa mjini Bujumbura nchini Burundi kwa mwaliko wa Shirika la Kijerumani la GIZ, ambapo Mtandao wa Wanafilamu wa Afrika Mashariki ulikuwa ukizinduliwa rasmi, sambamba na Tuzo za filamu kwenye Tamasha la Kimataifa la Filamu la Burundi (Festicab) 2014, linalofanyika jijini Bujumbura.



Kabla ya safari yangu hii, nilipata bahati ya kupitia nchi zingine kama mbili ambapo nilipata nafasi ya kukutana na watengeneza filamu wa nchi hizo, na kwa kweli nilijifunza mengi kutoka kwao.

Jun 16, 2014

HARAKATI ZA TAFF: Serikali, sikieni kilio chetu kwa mustakabali wa Taifa



Katibu Mkuu wa TAFF, Bishop Hiluka, akitoa ufafanuzi katika warsha ya wadau wa sanaa nchini, iliyofanyika kwenye hoteli ya Chichi, Kinondoni B, jijini Dar es Salaam hivi karibuni
 
HEBU jaribu kupata picha: umelima shamba lako na kupanda mahindi ambayo umeyatunza vizuri na yako tayari kuvunwa… unaamka siku moja na kukuta kuna mtu kayavuna na ameanzisha biashara inayompatia fedha nzuri wakati wewe uliyelima huna hata fedha ya kula! Au umenunua suti nzuri akaja mtu akaivaa harusini, kesho yake anakuja kukutaarifu jinsi walivyomsifia harusini kwa kupendeza na suti yako. Hiyo ndio picha ilivyo katika shughuli za sanaa Tanzania. Na haswa katika mambo ya filamu.

Katika mifano hii midogo moja kwa moja unapata picha halisi ya kile kinachoendelea kwenye tasnia ya filamu na hata sanaa zingine hapa nchini, ambayo tunaweza kuiita kuwa ni shamba la bibi, kwani kila anayejisikia anaingia, anavuna tani yake na kufaidi mazao pasipo kulima.

Jun 11, 2014

Wasanii wanajifunza nini kwenye vifo mfululizo vya wasanii wenzao?

Marehemu Said Ngamba maaruf kwa jina la Mzee Small



KWANZA naomba nianze kwa kutoa pole kwa familia nzima ya wasanii na wadau wa filamu nchini kufuatia vifo mfululizo vya wasanii wa filamu ndani ya wiki tatu; Adam Kuambiana, Rachel Haule, George Otieno “Tyson) na Said Ngamba maarufu kama Mzee Small. Mfululizo wa vifo hivi umeambatana na uvumi au dhana potofu inayosambaa kwa kasi, eti vifo mfululizo vya wasanii vinatokana na kafara inayofanywa na baadhi ya wadau (wasanii) ndani ya tasnia ya filamu kwa lengo fulani lenye maslahi kwao.

Uvumi huu umejitokeza hasa baada ya kushuhudia kundi la watu fulani likiwa ndiyo kinara wa kukumbatia misiba ya wasanii nyota, kuunda kamati mbalimbali na kuchangisha fedha nyingi ambazo baadhi yake zimekuwa zikitumika kununulia majeneza ya bei mbaya, vyakula vya gharama (utadhani kuna sherehe) na shughuli zingine ikiwemo ukodishaji wa magari ya kusindikiza msafara wakati wa mazishi. Lakini kama hiyo haitoshi, kumeripotiwa pia kufanyika kwa ubadhirifu wa pesa.

May 31, 2014

Kudumaa kwa Sekta ya Filamu Tanzania kunatokana na kukosa muongozo

Naibu Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Michezo, 
Juma Nkamia



Alhamisi wiki hii, Wizara ya habari, Vijana, Utamaduni na Michezo ilisoma bajeti yake ya mwaka 2014/15 na kuweka vipaumbele vyake. Lakini pamoja na kuigusa sekta ya filamu bado imekuwa haipewi kipaumbele japo imeonekana kuchangia kwa kiasi kikubwa katika ajira na pato la Taifa.

Tanzania ni moja ya nchi chache zenye maeneo mazuri ya kuvutia yanayofaa kabisa kwa kutengenezea filamu, ni nchi yenye wasanii wengi wazuri wenye vipaji lakini waliokosa muongozo. Tasnia ya filamu na muziki nchini ni sekta tajiri sana lakini zisizopewa kipaumbele.

May 14, 2014

Kwa hili la kukaa mezani na kuutazama upya mfumo unaofaa, naipa tano Serikali

Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba, akizungumza Bungeni


KATIKA jitihada za kuhakikisha kuwa wasanii hapa nchini Tanzania wanatengenezewa mazingira mazuri zaidi ya kufaidika na kazi wanazotengeneza, Serikali imetoa maagizo kwa Chama Cha Hatimiliki Tanzania, COSOTA na Mamlaka ya Mapato nchini, TRA, kukutana ndani ya siku tano za kazi kuanzia sasa. Mpango huu ni kwa ajili ya kutengeneza makubaliano juu ya mfumo utakaofaa kwa ajili ya kukusanya na kudhibiti mapato ili kuboresha faida kwa wasanii na serikali.



Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Mwigulu Nchemba, alitoa kauli hiyo bungeni ambapo alitaka waangalie namna ya kuboresha stempu/stika zinazobandikwa katika kazi za wasanii ili badala ya kutumika kukusanya ushuru peke yake zitumike pia kulinda kazi za wasanii hao.

Apr 30, 2014

Nollywood na mchango wa uchumi Nigeria, Tanzania na upuuzaji wa sekta ya hakimiliki

Desmond Eliot, msanii wa Nollywood

HIVI karibuni Nigeria imetangazwa kuwa ndilo Taifa lenye uchumi mkubwa barani Africa na kuipita Afrika Kusini. Pato Ghafi la Ndani (Gross Domestic Product ‘GDP’) la Nigeria limefikia Dola Billion 509 huku lile la Afrika ya Kusini likifikia Dola Bilioni 322.

Kwa mujibu wa Idara ya Takwimu ya Nigeria, Nigeria imekuwa Taifa lenye uchumi mkubwa Afrika baada ya wanauchumi wa nchi hiyo kuziongeza sekta za Mawasiliano na Filamu (Nollywood) kwenye takwimu. Ni dhahiri kuwa soko la Filamu la Nigeria linatoa mchango mkubwa mno katika ukuaji wa uchumi wa nchi hiyo. Kabla ya hapo Nigeria ilionekana kama taifa linalotegemea zaidi uuzaji wa mafuta na ilikadiriwa kuwa pato la mafuta lilichangia asilimia 32 kwenye GDP lakini ripoti ya wanauchumi hivi karibuni imeonesha sasa pato la mafuta huchangia Asilimia 15 tu ya pato ghafi la ndani.

Mar 25, 2014

MATOKEO YA UBINAFSI NA UMIMI: Msanii awabeza wasanii wenzake...

*Haya ni matokeo ya kupoteza dira kama Taifa
Viongozi wa Mashirikisho la Sanaa wakiwa pamoja na Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Paul Mtendah (wa pili kushoto) na Maria Sarungi (wa tatu kushoto), kwenye hoteli ya Dodoma, kabla ya vikao vya Bunge kuanza


WIKI iliyopita kwenye gazeti moja litolewalo kila siku (ambalo limetoka kifungoni hivi karibuni) kulikuwa na makala ya mwandishi mmoja ambaye pia ni msanii aliyesomea taaluma ya sanaa katika Taasisi ya Sanaa Bagamoyo, iliyobeza juhudi zinazofanywa na wasanii hivi sasa kupigania kutajwa kama mojawapo wa kundi muhimu kwenye Katiba ya nchi. Makala hayo yaliyojikita katika kile ambacho mwandishi huyu (nitamtaja zaidi kama msanii) alidai kuwa wasanii wenzake wamekumbuka shuka wakati kumekucha, kiasi cha kuzua mjadala mkubwa kwenye mtandao wa kijamii wa facebook.