Jun 6, 2013

KUELEKEA 1 JULAI 2013: Hivi tuna uhakika na mfumo wetu wa urasimishaji?

Sina hakika kama kuna nia ya dhati kumkomboa msanii


Wadau wa sanaa wakichangia mawazo yao kwenye Jukwaa la Sanaa linaloendeshwa kila Jumatatu na Basata

FILAMU zimeibuka kuanzia karne ya ishirini na baadaye kuwa kishawishi kikubwa na mawasiliano ghali katika karne ya ishirini na moja. Hakuna aina nyingine ya sanaa ambayo imesambaa kwa ufanisi na kuonekana kuvuka mipaka ya kiutamaduni katika mataifa mengi.


Katika karne hii, teknolojia ya televisheni na maonesho mbalimbali ya wajasiriamali vimeitangaza sana tasnia ya filamu kwa watu wote; watazamaji wa mijini na vijijini katika nchi nyingi zinazoendelea. Hata hivyo, filamu nyingi zinazosambazwa kimataifa na kupenya soko la nchi nyingi ni zile zinazozalishwa nchini Marekani na baadhi ya nchi za  Ulaya. Ukweli huu, pamoja na kutambua nguvu ya filamu “inayoyumbisha mioyo na akili za watu” unaamsha wasiwasi kwa walio wengi.

May 30, 2013

Vita ya bidhaa bandia ianze na maudhui






KWA siku za karibuni tumekuwa na mazungumzo ya kina kati Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF), Shirikisho la Wenye Viwanda Tanzania (CTI) na taasisi zingine kuhusu mpango-mkakati wa nam,naa ya kudhibiti bidhaa bandia na hafifu (counterfeit and substandard) zinazotishia uhai wa soko la kazi za Kitanzania zikiwemo kazi za sanaa (filamu na muziki).

Siku hizi imekuwa si jambo la ajabu kusikia au kushuhudia bidhaa kama nondo za ubora hafifu, betri, TV, mafeni, breki za gari, dawa nk. Jambo hili limekuwa likituumiza mno na sasa tumelishuhudia kwa kasi likivamia sekta ya sanaa kwa kiwango kikubwa na kutishia uhai wa soko la filamu na muziki, hasa kwenye bidhaa kama DVDs, CDs, Tape, Vifungashio (Packaging system) nk, ambazo zinahusiana moja kwa moja na sanaa la filamu. Inaudhi mno pale unaponunua sinema (DVD) unayotegemea kwenda kuangalia nyumbani lakini unapoiweka kwenye deki unaitazama mara moja tu, ukiirudia unagundua kuwa inakwama, na wakati mwingine hugoma hata kabla haijaangaliwa!

May 16, 2013

KILIO CHA WASANII KUIBIWA: Je, ni kweli msanii muigizaji ana hakimiliki?


Mmoja wa wasanii waigizaji nchini, Issa Mussa maaruf kwa jina la Claude

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Said Mwema

MAKALA yangu ya wiki iliyopita iliyohusu mikataba ya wasanii imezua maswali mengine kutoka kwa wasomaji wangu, hasa kutokana na maswali kadhaa niliyoyaibua kuhusu ile hoja ya kilio cha wasanii kulia kuibiwa kazi zao. maswali niliyoyaibua ni kama: Je, ni kweli wanaibiwa? Na kama wanaibiwa, huwa wanaibiwaje? Je, ni kweli uharamia (piracy) wa kazi za filamu ndiyo tatizo kubwa kwenye tasnia ya filamu nchini? Kama ni kubwa lipo kwa kiwango gani? Hivi, wasanii wanayafahamu kweli matatizo yao ya msingi?

Baadhi ya wasomaji wamenitaka niyatolee ufafanuzi maswali haya ili hata wao waelewe kwa kina kinachotokea kwani nimezidi kuwaacha gizani. Ndiyo maana wiki hii nimekuja na swali litakalosaidia kutafuta majibu ya maswali haya; je, ni msanii wa filamu ana hakimiliki?

May 9, 2013

Malalamiko ya wizi wa kazi za Sanaa: Tuwe na elimu endelevu kuhusu mikataba


Biashara ya filamu huambatana na matangazo kama inavyoonekana kwenye picha hii

MAPEMA wiki hii nilipata nafasi ya kuhudhuria warsha ya siku tatu ya wadau wa filamu iliyokuwa na lengo la kutafuta njia nzuri ya namna ya kutatua matatizo ya wasanii na wadau wa filamu badala ya tabia iliyojengeka ya kumtafuta mchawi jambo ambalo limekuwa halitusaidii.

Warsha ilitokana na kilio cha muda mrefu cha wasanii kudai kuibiwa kazi zao huku baadhi ya waliokuwa wakisukumiwa lawama wakiwa ni wamili wa maktaba za video na wenye mabanda ya kuoneshea video. Warsha hii pia ilikuwa na kusudio la kuangalia mzunguko wa biashara ya filamu nchini kuanzia inapotengenezwa hadi kumfikia mtu wa mwisho (mtazamaji). Warsha hii iliandaliwa na taasisi ya MFDI-Tanzania kwa lengo la kuangalia namna ya kutatua tatizo la usambazaji nchini.

Apr 11, 2013

Ili kudumisha maadili: Tuipe kipaumbele Idara ya Utamaduni


Mkurugenzi wa Utamaduni wa Wizara ya Habari, Vijana,
Utamaduni na Michezo, Prof. Hermas Mwansoko, akiongea
jambo katika moja ya shughuli za Idara yake

BAADA ya uhuru Disemba 1961, Serikali iliunda Wizara ya Utamaduni wa Taifa na vijana, mwaka 1962, Mwalimu Julius Nyerere alitamka wazi kuwa Utamaduni ni kiini na roho ya Taifa, nchi inayokosa utamaduni wake ni sawa na mkusanyiko wa watu usiokuwa na roho na hivyo kukosa sifa ya kuitwa taifa kamili.

Lakini chakushangaza pamoja na umuhimu uliopo katika suala la utamaduni kwa maisha ya watu, bado sera ya utamaduni imepewa nafasi finyu katika serikali yetu tangu ilipoanzishwa wizara ya kushughulikia masuala ya sanaa. Katika kipindi chote tangu mwaka 1962, shughuli za sanaa zilipewa nafasi katika mfumo wa kiserikali lakini zimekuwa hazithaminiwi.

Mar 28, 2013

Unauza haki yako ili iweje?


Aliyekuwa Afisa Mtendaji wa COSOTA, Yustus Mkinga

SIKU ya Jumanne ya tarehe 26 Machi 2013, ambayo kwangu ilikuwa siku muhimu sana kwani ndiyo siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwangu, siku hii nilipata maliko wa kuitwa kwenye kikao cha mazungumzo kati ya COSOTA na Viongozi wa Mashirikisho (Muziki, Stadi za Ufundi, Filamu), niliingia kwenye kikao hiki kwa mujibu wa nafasi yangu ya Ukatibu Mkuu wa Shirikisho la Filamu Tanzania.

Mazungumzo yetu yalikuwa na ajenda kadhaa ikiwemo kumtambulisha Afisa Mtendaji Mkuu mpya wa Cosota, baada ya aliyekuwepo kumaliza muda wake.

Jan 30, 2013

Kwa hili la Idara ya Utamaduni, tasnia hii itaendelea kuyumba


Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo,
Dk. Fenela Mukangara

SERIKALI imekuwa ikijinadi kuwa inawajali wasanii ndiyo maana imeamua kuutambua mchango wao kwa kuirasimisha tasnia ya burudani - hasa filamu na muziki – ili wasanii wafaidi jasho la kazi yao, na imekuwa ikionesha kwa vitendo kuwa karibu na wasanii pindi kunapotokea msiba wa msanii maarufu, ingawa bado kuna maswali kadhaa ambayo yanajitokeza na kuleta maswali makubwa zaidi kama kweli inawajali.

Inashangaza kuona kuwa Wasanii ambao Serikali inajigamba kuwajali hadi leo tunapojigamba kuingia kwenye urasimishaji bado hawana sera (ya filamu kwa waigizaji au ya muziki kwa wanamuziki) inayowaongoza katika kufikia mafanikio ya tasnia yao. Pia inashangaza kuona kuwa Idara muhimu ambayo ndiyo uti wa mgongo wa sanaa nchini, ya Utamaduni limekuwa tatizo jingine kubwa kwa mustakabali wa maendeleo ya sanaa nchini.