Sep 28, 2016

MAFUNZO KWA WAANDISHI: Pongezi kwa Bodi ya Filamu Tanzania

Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania, Joyce Fissoo, akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya Waandishi wa Filamu kwa baadhi ya waandishi hao Jijini Dar es Salaam hivi karibuni.

MWANDISHI mzuri wa filamu ni lazima awe na kipaji na uwezo mzuri wa kuandika. Kipaji mtu huzaliwa nacho au hukipata (adapt) katika umri mdogo kutokana na mazingira anayokulia. Uandishi mzuri wa filamu huanzia katika kuwa na uwezo wa kuumba maneno ambayo yatakuwa rahisi kueleweka pindi mtu akiyasikia.

Wakati unaandika ni muhimu sana kuzama ndani ya akili za walengwa wako ujue wanataka nini.

Sep 14, 2016

Tutumie filamu na nyimbo kuhamasisha uzalendo

Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Filamu, Bi Joyce Fisso
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo . Nape Nnauye akipata maelezo juu ya utamaduni wa kucheza bao kwenye kituo cha Utamaduni wa kisukuma Bujora
TUNAELEKEA kutimiza miaka 55 tangu tuwe huru, lakini bado jamii ya Kitanzania imeendelea kupoteza maadili, mila na tamaduni zake kila kukicha. Baada ya uhuru wa Tanganyika mwaka 1961, Wizara ya Utamaduni wa Taifa na Vijana iliundwa mwaka 1962, rais wa wakati huo, Mwalimu Julius Nyerere, ambaye alitamka wazi kuwa Utamaduni ndiyo kiini na roho ya Taifa, na nchi inayokosa utamaduni wake ni sawa na mkusanyiko wa watu usiokuwa na roho na hivyo kukosa sifa ya kuitwa taifa kamili.