Mar 30, 2016

Tunamisi burudani za majumba ya sinema

Watu wakiangalia sinema
LEO nimekumbuka mbali sana, hasa baada ya kupita sehemu na kuwasikia wanafunzi wa shule ya msingi (wenye miaka isiyozidi kumi), ambao wapenzi wa sinema, wakisimuliana na kubishana kuhusu kina Ray, Kanumba, Gabo nk. Ndipo nikakumbuka nilipokuwa katika umri huo tulikuwa pia tukisimuliana na kubishana kuhusu kina Amitabh Bachchan, Mithun Chakrabot, Amjad Khan, DharmendraSanjeev Kumar, Charlie Chaplin, nk.

Wakati huo hatukuwa na vituo vya televisheni kama leo. Vituo vya televisheni Tanzania Bara televisheni vimeanza mwanzoni mwa miaka ya 1990. Hadi 1996 kulikuwa na vituo vitatu tu vya CTN, DTV na ITV. Hata hivyo, televisheni imekuwapo Zanzibar tangu mwaka 1973.

Mar 2, 2016

LEONARDO DICAPRIO: Avumilia miaka 6 kushinda Tuzo ya Oscar


TUZO za Oscar (The Academy Awards), huwakilishwa kila mwaka na kampuni ya Academy of Motion Picture Arts and Sciences (Kifupi: AMPAS) kwa lengo la kutambulisha taaluma ya tasnia ya filamu, wakiwemo waongozaji, waigizaji, na watunzi wa filamu. Rasmi huwa sherehe za utoaji wa tuzo mbalimbali. Pia inasemekana kuwa ni miongoni mwa sherehe zinazotazamwa sana duniani mara tu sherehe hizo zinapoanza.

Katika Tuzo za mwaka huu mwigizaji nyota wa Hollywood, Leonardo DiCaprio, hatimaye amejishindia tuzo yake ya kwanza ya Oscar kwa uigizaji wake katika filamu ya ‘The Revenant’, baada ya kushindania tuzo hizo mara sita. Amekuwa mwigizaji bora kwenye Tuzo za 88 za Oscar.

Nani kaiua Sekta ya Filamu ya Tanzania?

Afisa kutoka Bodi ya Filamu Tanzania, Wilhad Tairo, akifafanua jambo kwa mfanyabiashara wa duka la Filamu wakati wa Operesheni ya kukagua Bidhaa zisizo na stika za TRA
Mwenyekiti wa Bodi ya Filamu Tanzania, Sylvester Sengerema

HALI ya Sekta ya Filamu ya Tanzania kwa sasa ni mbaya sana. Ninathubutu kusema kwamba sekta hii ipo ukingoni mwa kifo, kilichobaki ni ung’ang’anizi tu. Ikumbukwe kuwa mzunguko wa maisha hufuata hatua nne: kuzaliwa, kukua, kukomaa na kuzeeka kabla ya kifo, ambapo kama hakuna matatizo, tunategemea mwanadamu kufa baada ya hatua hizo.