Oct 21, 2015

WITO KWA WASANII: Kuna maisha hata baada ya uchaguzi

Baadhi ya wasanii wa Filamu wakiwa kwenye uzinduzi wa Kampeni za mgombea Urais wa Chadema anayeungwa mkono na UKAWA, Edward Lowassa
MWAKA HUU ninashuhudia mihemko ya ajabu ya kisiasa kwa wasanii kushabikia siasa na wanasiasa! Kwa mara nyingine tena nashuhudia namna wasanii wa fani mbalimbali wanavyodhihirisha umuhimu wao katika kipindi hiki cha uchaguzi mkuu, wakihusika katika kampeni za vyama, na kwa wagombea wa ngazi tofauti.

Nilipoona mihemko hii nilijiuliza kama kuna manufaa yoyote wanayopata kwa kushiriki kampeni hizi? Jibu likawa, yapo, kwani hiki ni kipindi cha mavuno kwa wasanii.

Je, unajua kuwa Filamu ya Yesu imerudiwa upya?

Muigizaji wa filamu ya Yesu, Brian Deacon

TAKRIBAN baada ya miaka 35 tokea sinema ya Yesu iliyoigizwa na Brian Deacon, muigizaji ambaye watu wengi wa kizazi cha siku hizi huamini kuwa ndiye Yesu, imerudiwa tena katika mfumo wa hali ya juu, kuanzia picha na hata uchanganyaji wa sauti.

Jesus, filamu ambayo ndiyo imevunja rekodi na inaongoza duniani kwa kutafsiriwa kwenda lugha nyingi, kwani kwa mujibu wa kitabu cha kumbukumbu cha Guiness, (Guiness World Record) filamu hiyo imetafsiriwa kwenda lugha 1,197 tofauti duniani kote, na kutazamwa na zaidi ya mara bilioni moja, huku watu zaidi ya milioni mbili wakiokoka kutokana na kutazama sinema hiyo.

Oct 7, 2015

KAMPENI 2015: U wapi uchumi na utajiri wa wasanii? - 2

Wasanii wa filamu, Anti Ezekiel na Jackline Wolper,
wakiunga mkono siasa za Chadema
Msanii wa vichekesho, Steven Mengere (Steve Nyerere),
katika mikutano ya CCM
WIKI HII nimelazimika kuendeleza mjadala wa ‘uchumi na utajiri wa wasanii’, hasa baada ya baadhi ya wasomaji wangu kunitumia ujumbe kutaka ufafanuzi katika mambo fulanifulani. Hata hivyo, wengi wao wanakubaliana na hoja yangu kwamba sanaa siyo sekta ya kuchezewachezewa, wala haipaswi kupuuzwa hata kidogo na wanasiasa wetu.