Sep 30, 2015

KAMPENI 2015: U wapi uchumi na utajiri wa wasanii?

Wasanii waliopo katika kampeni ya Mama Ongea na Mwanao mpigie kura Dk. Magufuli
KAMPENI za Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu zimepambwa zaidi na wasanii mbalimbali. Kumekuwepo na mhemuko wa ajabu wa wasanii kujitokeza kwenye majukwaa ya siasa, wengi wao wakijipambanua kuwa wafuasi au mashabiki wa vyama na wanasiasa fulani. Zikiwa zimesalia siku 22 tu kabla ya kupiga kura kuichagua serikali ijayo (Rais, Wabunge na Madiwani), hali bado ni ya mashaka kwa sekta ya sanaa.

Wasanii wanatumika kwa kiasi kikubwa kwenye majukwaa ya siasa, kiasi cha mikutano kugeuka kuwa matamasha ya burudani, huku wakiwa hawajui majaliwa yao kuhusu ustawi wa sekta ya sanaa, zaidi ya kupigwa porojo na ahadi zisizotekelezeka.

Sep 16, 2015

Sekta ya filamu Tanzania imekosa uhalisia


KATIKA wasanii mastaa ambao wangepaswa kuishi maisha mazuri hapa Tanzania, wasanii wa filamu ndiyo wangepaswa kuwa wanashikilia chati za juu kutokana na jinsi kazi zao zinavyotengeneza fedha nyingi. Kwa mujibu wa takwimu, kazi za wasanii hao zimekuwa zikiingiza fedha nyingi tofauti na ilivyokuwa awali, lakini maslahi hayo hutofautiana kwani wapo baadhi ambao hawashikiki.

Sep 9, 2015

Tuache utengenezaji sinema wa kulipuwa


SEKTA YA FILAMU nchini imekuwa inakua kwa kasi na kuwa kimbilio la vijana wengi, hata wale walioshindwa (failures) katika sekta zingine. Ukuaji wake umeambatana na changamoto nyingi katika kufikia ubora unaokubalika kimataifa kwenye filamu zetu.

Filamu ni nguzo muhimu sana ya Utamaduni wa nchi. Filamu zimeibuka kuanzia karne ya ishirini na baadaye kuwa kishawishi kikubwa na mawasiliano ghali katika karne ya ishirini na moja. Hakuna aina nyingine ya sanaa ambayo imesambaa kwa ufanisi na kuonekana kuvuka mipaka ya kiutamaduni katika mataifa mengi kama hii.