Jun 29, 2015

“Spec Scriptwriting”, uandishi wa filamu wenye changamoto nyingi

Waandishi mahiri wa script Tanzania, Dk.Vicensia Shule na
Bishop Hiluka, katika moja ya mikutano ya Bodi ya Filamu
Ikiwa una matumaini kuwa siku moja utakuja kufanya kazi ya uandishi wa script kwa ajili ya filamu au televisheni, basi unahitaji kuwa na ufahamu wa jinsi ya kuandika “spec” script. Spec Script ni kifupi cha Speculative script, huu ni uandishi wa filamu wa kubahatisha (speculation), ambao kama mwandishi unaandika script yako ukiwa hujui nani atakuja kutumia script hiyo – hii humaanisha kuwa unaandika script bure (pasipo kulipwa au kuajiriwa na mtu). Kwa maana nyingine ni kwamba hakuna mtu aliyekuajiri au anayekulipa kuandika script hiyo. 

Unaandika ukiwa na matumaini ya kuja kuuza kwa mnunuzi yeyote atakayevutiwa na kisa chako au kuajiriwa kwa ajili ya kuandika script kwa sababu ya hiyo, lakini ili kuwa na nafasi au uwezekano, huna uchaguzi bali kuandika spec script.

Jun 22, 2015

Sekta ya televisheni na mchango wa utamaduni

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Prof. Elisante Ole Gabriel, akikata utepe kuzindua Tamthilia ya 'Doudou na Wakwe Zake' katika Viwanja vya TBC mwaka 2014
SEKTA ya Televisheni nchini kwa sasa imekuwa ni sehemu muhimu sana ambayo haiwezi kukosekana katika maisha ya kila siku ya mwananchi, iwe mwananchi huyo anamiliki seti ya televisheni au la. Kwa kutazama vipindi mbalimbali vya televisheni mtu huweza kufahamu mambo mengi makubwa yanayoendelea nchini na hata nchi za nje, na kwa kutazama televisheni unapata burudani za kila aina.

Japo sekta ya televisheni nchini inakabiliwa na fursa nzuri ya maendeleo kutokana na dunia kuingia zama za dijitali lakini pia ina changamoto kubwa. Kwa upande mmoja, maendeleo ya haraka ya dijitali yameiletea sekta hiyo fursa nzuri ya kujiendeleza, na kwa upande mwingine, aina za uenezi wa habari zimekuwa nyingi, kwa mfano, televisheni kwenye mtandao wa internet, simu za mkononi zinaendelea haraka na makundi mengi ya televisheni ya nchi za nje yameingia kwenye soko la televisheni nchini, hali kama hiyo imekuwa shinikizo kubwa kwa sekta ya televisheni na filamu nchini.

Jun 17, 2015

Sekta ya Filamu duniani inahodhiwa na Wayahudi

Mtengeneza filamu wa Hollywood, Steven Spielberg
KATIKA zama zetu hizi, sinema ni chombo muhimu sana kinachotumiwa kueneza utambulisho, utamaduni na fikra. Mfano maalumu wa uwekezaji mkubwa katika sekta ya sinema duniani ni uwekezaji wa Wamarekani na Waisrael (Wayahudi) katika sekta ya filamu. Wakati wengine wamelala, Wayahudi walifahamu mapema sana taathira ya sekta ya sinema na umuhimu wake katika propaganda na ili kuidhibiti sekta hii walitumia uwezo wao wote.

Katika miaka ya karibuni Serikali ya Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran wameonekana kuanza kuzinduka katika usingizi na kuanza kujipenyeza kwenye sekta ya filamu duniani ili kueneza utambulisho na tamaduni za Kiislamu dhidi ya tamaduni za Kimagharibi, lakini bado wana kazi ngumu sana kufuta alama zilizoachwa na sinema za Hollywood, chini ya udhibiti wa Israel na Marekani.

Waraka wa Bond Bin Sinnan, kwa Wasanii wa filamu Tanzania

Abdulrazaq Sinnan, maarufu kama Bond Bin Sinnan
Wasanii wa Bongo Movie wakiwasalimia wananchi waliojitokeza kumsikiliza Waziri wa Mambo ya Nje, Bernard Membe, wakati wa kutangaza nia ya kugombea Urais kupitia CCM
Jina langu naitwa Abdulrazaq S.H. Sinnan ingawa asilimia kubwa ya Watanzania wananifahamu kwa jina la Bond Bin Sinnan kwa takribani miaka 15 sasa najishughulisha na masuala ya tasnia ya filamu nikiwa kama mtunzi, muigizaji, mzalishaji na muongozaji wa filamu. Hivyo nina upeo na uzoefu mkubwa wa tasnia ya filamu Tanzania. Naijua faida yake, matatizo yake na mengine mengi yanayoihusu tasnia hii.

Kwanza nianze kwa kuwapongeza sana wasanii wenzangu wa filamu nchini kutokana na kujituma kwetu mpaka tumefanya tasnia hii kuwa ajira kubwa kwa watanzania wengi sana. Vilevile tasnia hii imekuwa ni burudani kubwa kwa wana Afrika Mashariki na Kati kwani zaidi ya watu milioni kumi wanaangalia filamu za Kitanzania.

Jun 12, 2015

Sekta ya filamu inaendeleza ubaguzi dhidi ya wanawake


Mmoja wa waigizaji maaruf wa sinema za Hollywood, Angelina Jolie
Ripoti moja ya utafiti wa kwanza kufanyika duniani kuhusu wahusika wa kike katika filamu, umebainisha kuwa ubaguzi wa wanawake na wasichana umeenea mno katika sekta hiyo ya filamu. Ripoti hiyo iliyozinduliwa mwezi Septemba mwaka jana imetokana na utafiti ulioidhinishwa na taasisi ya Geena Davis kuhusu Jinsia katika vyombo vya habari, ikisaidiwa na Shirika linalohusika na masuala ya wanawake, UN Women, pamoja na Wakfu wa Rockefeller.

Sir Christopher Lee, nyota wa filamu ya Dracula afariki

Moja ya scene alizocheza hayati Christopher Lee
Sir Christopher Lee
Mwigizaji wa siku nyingi na nyota wa filamu zilizopendwa na wengi, Sir Christopher Lee, amefariki akiwa na umri wa miaka 93. Msanii huyo ambaye jina lake kamili ni Christopher Frank Caradini Lee alizaliwa mnamo mwaka 1922, alikuwa mwigizaji wa filamu na mchekeshaji mzaliwa wa Uingereza aliyejenga jina lake kwa kuigiza katika filamu ya Dracula na Frankenstein katika filamu ya kutisha aligiza katika zaidi ya filamu 250.

Jun 10, 2015

Hadhi ya Sekta ya Filamu Tanzania

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na marehemu Steven Kanumba
KUMEKUWEPO mjadala kama hali ya sasa katika soko la filamu linaweza kuitwa ‘sekta rasmi’ ambapo mitaji, mitambo na rasilimali zipo kila mahali. Hakuna maendeleo yoyote yatakayopatikana pasipo uwepo wa Sera ya Filamu. Sera ya Filamu ni hati nzuri inayoandaa mazingira mazuri kwa ajili ya uzalishaji wa filamu na masoko.

Ni hati kuhusu hadhi na thamani ya sekta inayoonesha kutokosekana kwa miongozo ya lazima na visheni, inayotambua kuwa Filamu ni njia ya kipekee ya mawasiliano, ni njia ya kuelimisha na kuburudisha, inayotuweka pamoja, kupashana habari na kuhamasishana.

Jun 6, 2015

Makundi mapya ya sanaa za maigizo yajirekebishe

Wasanii wa Kundi la Sanaa la ABY, Malapa Buguruni
Jacob Steven maaruf kwa jina la JB
Ni wazi kwamba huwezi kuzungumzia maendeleo yaliyopatikana kwenye tasnia ya filamu nchini bila kutaja Nyota Academia, Kaole Sanaa Group, Kidedea, Kidedea Original, Mambo Hayo na makundi mengine ya sanaa za maigizo.

Kimsingi makundi haya ndiyo yaliwaibua wasanii wakubwa nchini kama marehemu Steven Kanumba, Vicent Kigosi (Ray), Jacob Stephen (JB), Yvonne Cherry (Monalisa), Blandina Chagula (Johari), Jengua na wengine wengi ambao wanaendelea kuipeperusha vyema bendera ya filamu za Bongo ndani na nje ya Tanzania.

Jun 5, 2015

Hiroshi Koizumi, mwigizaji wa filamu za Godzilla afariki dunia akisumbuliwa na homa ya mapafu

Hiroshi Koizumi, enzi za uhai wake
Moja ya sinema za Godzilla
Hiroshi Koizumi, msanii wa Japan ambaye aliigiza katika filamu nyingi za Godzilla amefariki akiwa na umri wa miaka 88. Kulingana na ripoti, alifariki mjini Tokyo tarehe 31 Mei 2015, kutokana na homa ya mapafu (Pneumonia) katika hospitali ya Tokyo.

Koizumi aliigiza kama Godzilla katika filamu ya ‘Godzilla Raids Again’ ikiwa ni filamu ya kwanza ya Godzilla. Baadaye aliigiza katika filamu kadhaa za kutisha ikiwemo ‘Mothra’, ‘Godzilla vs The Thing’ na ‘Ghindorah and the Three headed Monster’.

Jun 3, 2015

Mitandao ya kijamii inaweza kuwa darasa muhimu sana kwa wanataaluma

Baadhi ya waandishi wa Skripti wanaounda "Scriptwriters Club", 
walipokutana kujadili changamoto zinazowakabili. Mwandishi wa 
makala haya, Bishop Hiluka (nyuma ya mwenye shati nyekundu) 
ni mmoja wao
MIMI ni shabiki mkubwa wa mitandao ya kijamii, hususan Facebook, Twitter, YouTube nk. napenda kutumia mitandao hii ili kutafuta taarifa mpya na ku-share uelewa wangu (knowledge). Mitandao ya kijamii ni nyenzo muhimu ya kutuunganisha na watu – aidha kusikia au kutaka kusikika. Natambua nguvu ya mitandao ya kijamii katika kufikisha ujumbe, na huwa nafanya kila niwezalo kuitumia ili kufikisha sauti yangu isikike na hatimaye kuleta tofauti inayokusudiwa. 

Lakini tofauti na hivi, wengi hawaitumii mitandao hii ipasavyo, ndiyo maana mimi si shabiki wa makundi (groups) yaliyopo kwenye mtandao wa WhatsApp, si shabiki kwa kuwa makundi mengi ya WhatsApp ni kama vijiwe vya porojo, hayana dira wala malengo, mara nyingi kinachofanyika ni kupiga porojo zisizo na maana.