Nov 26, 2014

Uandishi bora wa Filamu: Tuanze kuwafundisha watoto jinsi ya kuandika script

Magdalena Hiluka, akiwa na miaka 4 wakati huo. Inashauriwa 
kumpa hamasa mtoto katika umri mdogo ili kujenga kipaji chake 


Tangazo (poster) la filamu ya Mke Mchafu.

NIANZE makala yangu kwa kumpongeza Mtayarishaji na Muongozaji wa filamu nchini, John Lister Manyara, kwa sinema yake “MKE MCHAFU” ambayo ni sinema pekee ya Tanzania iliyokubalika kuoneshwa kwenye ndege za Shirika la Ndege la Emirates. Haya ni mafanikio makubwa. Sinema hii imewashirikisha waigizaji maaruf wa Tanzania; Zuberi Mohammed (Niva), Hisan Muya (Tino) na Blandina Chagula (Johari) na wengineo, imeongozwa na John Lister na mimi (Bishop Hiluka) ndiye niliyeiandika. Mafanikio ya sinema hii yananihusu kwa kiasi kikubwa.

Nov 7, 2014

TAFA AWARDS: TUZO KUBWA ZA FILAMU TANZANIA



Logo ya Tuzo za Filamu Tanzania (TAFA)
Shirikisho la Filamu Tanzania kwa kushirikiana na kampuni ya Binary & Pixels wameanzisha Tuzo za Filamu nchini Tanzania zinazotazamiwa kuwa Tuzo kubwa zaidi kuwahi kutolewa. Kuanzia 1 Novemba hadi 30 Novemba 2014 ni kipindi cha watayarishaji na wasanii kutuma/kupeleka kazi zao kwa ajili ya kuwania Tuzo hizi. Fomu zinapatikana kwenye ofisi za TAFF au kwenye website ya Shirikisho hili: GONGA HAPA