Oct 18, 2014

Uongozaji si kujua ‘action’ na ‘cut’ tu, unatakiwa pia kuijua lugha ya filamu



Mmoja wa waongozaji filamu nchini, Issa Mussa maaruf kama Cloud 112

SINEMA za mwanzo zilijielekeza kama vile sehemu ya jukwaa mbele ya pazia. Kamera iliwekwa katika sehemu moja na matendo yote katika tukio zima yalifanyika ndani ya fremu hiyo ya kamera kwa pigo moja (one shot). Mtazamo wa watazamaji enzi hizo haukutofautiana na watazamaji ambao leo wanakaa mbele ya jukwaa wakiangalia mchezo wa kuigiza wa jukwaani.

Muongozaji wa Kimarekani, D. W. Griffith, ndiye alikuwa wa kwanza kuwahamishia watazamaji katika ulingo wa sinema kwa kazi zake kama “For Love of Gold (1908)”, “The Lonely Villa (1909)”, “The Lonedale Operator (1911)”, na ile iliyovutia zaidi, “Birth of a Nation (1915)”. Grifftith alikuja na mbinu kabambe za kuwafanya watazamaji kuwa sehemu ya hadithi zake.

Siku hizi tuna vichekesho au mizaha?


Wachekesha maaruf nchini, marehemu Hussein Mkiety (Sharomilionea) na Amri Athuman maaruf KIng Majuto



NILISHANGAA binti yangu, Magdalena, 10, aliposema siku hizi hapendi kuangalia comedy za Tanzania akidai hazichekeshi. Comedy ni neno la Kiingereza lenye asili ya Ugiriki likimaanisha futuhi au ucheshi kwa Kiswahili. Ni vichekesho vyenye lengo la kufurahisha, kufundisha na kuburudisha watazamaji, katika televisheni, filamu, na kwenye majukwaa. Unapocheka ndivyo maisha yanavyokua bora zaidi!

Ucheshi ni mwanga unaouangazia moyo, ni igizo lililobuniwa kuchekesha, kuburudisha, na kumfanya mtu astarehe. Muundo wa ucheshi ni kuzidisha hali ya mambo ili kuleta uchekeshaji, kwa kutumia lugha, matendo, na hata wahusika wenyewe. Ucheshi huhoji na kufuatilia yalipo mapungufu, makosa au hitilafu, na vitu vinavyokatisha tamaa ya maisha, na kuleta uchangamfu na wasaa wa kufurahia maisha.