· Wengi hawana sifa zinazohitajika na hawataki kujifunza
UKWELI tuna tatizo kubwa kwenye tasnia ya filamu Tanzania
kwa waongozaji wengi kudhani kuwa kazi ya uongozaji wa filamu ni kujua: “standby...
action... cut!” na kusahau kuwa muongozaji ndiye anayepaswa kumtengeneza
muigizaji aweze kuuvaa uhusika ipasavyo kwa kutegemea script ilivyo. Kama
muigizaji atashindwa kuvaa uhalisia, mara nyingi hilo siyo kosa lake bali ni
kosa la muongozaji kwa kushindwa kumtengeneza, na hutafsiri uwezo wa muongozaji
ulipokomea.
Mtazamo wangu, mtu yeyote
anayetaka kuwa muongozaji mzuri wa filamu katika tasnia yetu anapaswa kujifunza
kwa makini hatua kwa hatua kwa kusoma machapisho na kuhudhuria warsha na
mafunzo ya muda mfupi — si kwa ajili ya kujifunza njia nzuri ya utengenezaji wa
filamu, bali kwa ajili ya kupata msukumo wa kufuatilia masuala muhimu ya
uumbaji wa kisanii kwa bidii na kwa umakini.