Aug 21, 2014

Filamu zetu zinaharibiwa na waongozaji


·         Wengi hawana sifa zinazohitajika na hawataki kujifunza




UKWELI tuna tatizo kubwa kwenye tasnia ya filamu Tanzania kwa waongozaji wengi kudhani kuwa kazi ya uongozaji wa filamu ni kujua: “standby... action... cut!” na kusahau kuwa muongozaji ndiye anayepaswa kumtengeneza muigizaji aweze kuuvaa uhusika ipasavyo kwa kutegemea script ilivyo. Kama muigizaji atashindwa kuvaa uhalisia, mara nyingi hilo siyo kosa lake bali ni kosa la muongozaji kwa kushindwa kumtengeneza, na hutafsiri uwezo wa muongozaji ulipokomea.

Mtazamo wangu, mtu yeyote anayetaka kuwa muongozaji mzuri wa filamu katika tasnia yetu anapaswa kujifunza kwa makini hatua kwa hatua kwa kusoma machapisho na kuhudhuria warsha na mafunzo ya muda mfupi — si kwa ajili ya kujifunza njia nzuri ya utengenezaji wa filamu, bali kwa ajili ya kupata msukumo wa kufuatilia masuala muhimu ya uumbaji wa kisanii kwa bidii na kwa umakini.