May 31, 2014

Kudumaa kwa Sekta ya Filamu Tanzania kunatokana na kukosa muongozo

Naibu Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Michezo, 
Juma Nkamia



Alhamisi wiki hii, Wizara ya habari, Vijana, Utamaduni na Michezo ilisoma bajeti yake ya mwaka 2014/15 na kuweka vipaumbele vyake. Lakini pamoja na kuigusa sekta ya filamu bado imekuwa haipewi kipaumbele japo imeonekana kuchangia kwa kiasi kikubwa katika ajira na pato la Taifa.

Tanzania ni moja ya nchi chache zenye maeneo mazuri ya kuvutia yanayofaa kabisa kwa kutengenezea filamu, ni nchi yenye wasanii wengi wazuri wenye vipaji lakini waliokosa muongozo. Tasnia ya filamu na muziki nchini ni sekta tajiri sana lakini zisizopewa kipaumbele.

May 14, 2014

Kwa hili la kukaa mezani na kuutazama upya mfumo unaofaa, naipa tano Serikali

Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba, akizungumza Bungeni


KATIKA jitihada za kuhakikisha kuwa wasanii hapa nchini Tanzania wanatengenezewa mazingira mazuri zaidi ya kufaidika na kazi wanazotengeneza, Serikali imetoa maagizo kwa Chama Cha Hatimiliki Tanzania, COSOTA na Mamlaka ya Mapato nchini, TRA, kukutana ndani ya siku tano za kazi kuanzia sasa. Mpango huu ni kwa ajili ya kutengeneza makubaliano juu ya mfumo utakaofaa kwa ajili ya kukusanya na kudhibiti mapato ili kuboresha faida kwa wasanii na serikali.



Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Mwigulu Nchemba, alitoa kauli hiyo bungeni ambapo alitaka waangalie namna ya kuboresha stempu/stika zinazobandikwa katika kazi za wasanii ili badala ya kutumika kukusanya ushuru peke yake zitumike pia kulinda kazi za wasanii hao.