Oct 30, 2013

Wasomi wetu na kisa cha ‘Heri mimi sijasema’!


Wasomi kama hawa ni tegemeo katika jamii yetu, wanapokwepa majukumu yao kama wasomi ni hasara kwa taifa

NILIPOKUWA mdogo, moja ya sababu kubwa iliyonifanya nipende sana kwenda shule ni kusoma na kusikia hadithi na visa mbalimbali, ama kwa kuvisoma kwenye vitabu (wakati huo kila shule ilikuwa na maktaba yenye vitabu vya kutosha), au masimulizi kutoka kwa walimu wenye kupenda kufundisha kwa mifano. Hadithi nilizozisikia na kuzisoma zilijaa mafunzo ya kila aina, hadithi kama zile za kina Juma na Roza, Bulicheka na mke wake Elizabeth na Wagagagigikoko, au ile hadithi maaruf ya ‘Heri mimi sijasema’.

Hii ni hadithi iliyohusu vita katika ufalme fulani, ambapo wapiganaji watatu wakiwa vitani waliamua kujificha kwa kujifunika na nyasi, bahati mbaya adui akawa anapita eneo lile na kuwakanyaga bila kujua. Mmoja wa wapiganaji hao akalalamika; “kwanini unawakanyaga wenzio kama nyasi?” Yule adui akashtuka kuwa pale kuna mtu kajificha akamchoma mkuki na kumuua.

Oct 17, 2013

MMOMONYOKO WA MAADILI: Tutumie filamu, nyimbo zetu kuhamasisha uzalendo


Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, 
Dk. Fenella Mukangara

Niliwahi kuandika makala hii kuhusu kutumia filamu kuhamasisha uzalendo, nalazimika kuirudia kutokana na sababu fulanifulani ingawa ikiwa imeboreshwa zaidi.

Mwaka huu tarehe 9 mwezi Disemba tunatimiza miaka 52 tangu tuwe huru, huku tukishuhudia jamii ya Kitanzania ikizidi kupoteza maadili, mila na tamaduni zake kila kukicha. Baada ya uhuru wa Tanganyika mwaka 1961, Wizara ya Utamaduni wa Taifa na Vijana iliundwa mwaka 1962, rais wa wakati huo, Mwalimu Julius Nyerere, ambaye alitamka wazi kuwa Utamaduni ndiyo kiini na roho ya Taifa, na nchi inayokosa utamaduni wake ni sawa na mkusanyiko wa watu usiokuwa na roho na hivyo kukosa sifa ya kuitwa taifa kamili.

Oct 10, 2013

UTEKETEZAJI WA KAZI FEKI ZA SANAA: Ni kweli tunasaidia kumpoza msanii aliyeibiwa?



·        Tuzipitie upya sheria zetu za Hakimiliki

Maofisa wa Cosoza wakiteketeza CD na Mikanda ya wizi katika uwanda wa Kikungwi, Wilaya ya Kusini Unguja

“MWANAHARAKATI, kwanza kabisa nakushukuru sana kwa makala yako wiki hii, pili nakubaliana kabisa na wewe kuhusu ulichoandika kuhusu ‘matumizi ya muziki ni muhimu sana kwenye filamu zetu’. Ukweli ni kwamba suala la wasanii wetu kupenda kutumia nyimbo ambazo wala hawajaomba ruhusa kuzitumia ni jambo baya sana. Huu ni ukiukwaji mkubwa wa sheria za Hakimiliki, haina tofauti na ambavyo wao wamekuwa wakilalamika kuibiwa kazi zao, kwani hata wao ni wezi wa kazi za wengine.

Oct 3, 2013

Muziki ni muhimu sana kwenye filamu zetu

  • Watayarishaji wa filamu nchini hawana bajeti ya muziki
  • Wengi huokoteza miziki isiyoendana na maudhui

Kwenye nchi zingine wanamuziki kama hawa (John Kitime), wenye ubunifu huwa wanatumika kunogesha filamu kutokana na midundo ya muziki

WIKI hii nilitembelea ofisi ya watayarishaji wa filamu nchini, John Lister na Paul Mtendah, kwa lengo la kuwajulia hali, niliwakuta wakikamilisha uhariri wa sinema inayotazamiwa kutoka hivi karibuni ya ‘Mke Mchafu’, iliyotokana na mwongozo (script) niliouandika. Nikiri tu kuwa pamoja na kuandika script hiyo, lakini nilijikuta nikiangalia sinema ambayo ni kama vile sikuwahi kuiona hadithi yake kutokana na jinsi sauti na miziki iliyotumika kwenye filamu hiyo jinsi ilivyoleta radha tofauti.

Ingawa nilikuwa na haraka, nilijikuta navutiwa sana kuiangalia sinema kutokana na miziki iliyotumika kwenye sinema hiyo kuendana sana na matukio ya sinema na kukoleza mshawasha wangu wa kutaka kuiangalia hadi mwisho. Niliwadadisi watayarishaji hao kama miziki hiyo ilikuwa imetungwa maalum kwa ajili ya filamu hiyo au imetokea kama ajali (accidentally) tu.