Wasomi kama hawa ni tegemeo katika jamii yetu, wanapokwepa majukumu yao kama wasomi ni hasara kwa taifa
NILIPOKUWA mdogo, moja ya
sababu kubwa iliyonifanya nipende sana
kwenda shule ni kusoma na kusikia hadithi na visa mbalimbali, ama kwa kuvisoma
kwenye vitabu (wakati huo kila shule ilikuwa na maktaba yenye vitabu vya
kutosha), au masimulizi kutoka kwa walimu wenye kupenda kufundisha kwa mifano. Hadithi
nilizozisikia na kuzisoma zilijaa mafunzo ya kila aina, hadithi kama zile za
kina Juma na Roza, Bulicheka na mke wake Elizabeth
na Wagagagigikoko, au ile hadithi maaruf ya ‘Heri mimi sijasema’.
Hii ni hadithi iliyohusu
vita katika ufalme fulani, ambapo wapiganaji watatu wakiwa vitani waliamua
kujificha kwa kujifunika na nyasi, bahati mbaya adui akawa anapita eneo lile na
kuwakanyaga bila kujua. Mmoja wa wapiganaji hao akalalamika; “kwanini
unawakanyaga wenzio kama nyasi?” Yule adui
akashtuka kuwa pale kuna mtu kajificha akamchoma mkuki na kumuua.