Aug 7, 2013

Uongozaji huu wa filamu utaleta maafa makubwa


 Muigizaji wa filamu Tanzania, Maulid Mfaume, aliyevunjika miguu yote kwa kujirusha toka ghorofa ya nne wakati wa upigaji picha

UONGOZAJI wa filamu ni zaidi ya kujua “standby... action... cut!” Uongozaji wa filamu ni tatizo kubwa mno kwenye tasnia ya filamu nchini, ni tatizo kwa kuwa waongozaji wetu wa filamu hudhani kuwa kazi ya uongozaji wa filamu ni kujua “standby... action... cut!” na kusahau kuwa muongozaji wa filamu anapaswa kuwa mbunifu na kiungo muhimu kati yake na timu ya uzalishaji.

Muongozaji wa filamu anawajibika kuutafsiri muongozo wa filamu ulioandikwa kwenye karatasi na kuuhamishia katika picha halisi na sauti kwenye skrini – na anapaswa kuiona taswira halisi na kutafsiri mtindo na muundo wa filamu hiyo, na hivyo kufanya kazi zote mbili kama kiongozi wa timu na msimulizi kwa kutoa picha halisi. Pia anapaswa kuangalia mtu anayefaa kuigiza, ndiyo maana mojawapo ya majukumu ya muongozaji ni pamoja na kufanya usaili (casting).

Aug 1, 2013

Utamaduni wa Mtanzania: Ni nani wenye dhamana ya kutoa tafsiri sahihi?


  • Walioaminiwa wanatupoteza, sasa hatuna mwelekeo

Huu ndiyo utamaduni wa Kiafrika unaopingana na tafsiri ya wakubwa


“UTAMADUNI wa Mtanzania, are we sure?” nilijikuta nikitupiwa swali na jamaa yangu mmoja kwa utani baada ya kusoma makala yangu moja iliyokuwa na kichwa cha habari: “Kupuuzwa kwa Utamaduni: Hii ndo fursa ya wasanii kuchangia maoni yao kwenye rasimu ya Katiba mpya”.

Nilimtazama kwa mshangao nikiwa sielewi alichokuwa akimaanisha. Alitabasamu na kuketi kando yangu akiwa kashika gazeti, nikalitupia jicho na kuuona ukurasa aliuokuwa akiusoma.