Aliyekuwa Afisa Mtendaji wa COSOTA, Yustus Mkinga
SIKU ya Jumanne ya tarehe
26 Machi 2013, ambayo kwangu ilikuwa siku muhimu sana kwani ndiyo siku ya
kumbukumbu ya kuzaliwa kwangu, siku hii nilipata maliko wa kuitwa kwenye kikao
cha mazungumzo kati ya COSOTA na Viongozi wa Mashirikisho (Muziki, Stadi za
Ufundi, Filamu), niliingia kwenye kikao hiki kwa mujibu wa nafasi yangu ya
Ukatibu Mkuu wa Shirikisho la Filamu Tanzania.
Mazungumzo yetu yalikuwa na
ajenda kadhaa ikiwemo kumtambulisha Afisa Mtendaji Mkuu mpya wa Cosota, baada
ya aliyekuwepo kumaliza muda wake.