Mar 28, 2013

Unauza haki yako ili iweje?


Aliyekuwa Afisa Mtendaji wa COSOTA, Yustus Mkinga

SIKU ya Jumanne ya tarehe 26 Machi 2013, ambayo kwangu ilikuwa siku muhimu sana kwani ndiyo siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwangu, siku hii nilipata maliko wa kuitwa kwenye kikao cha mazungumzo kati ya COSOTA na Viongozi wa Mashirikisho (Muziki, Stadi za Ufundi, Filamu), niliingia kwenye kikao hiki kwa mujibu wa nafasi yangu ya Ukatibu Mkuu wa Shirikisho la Filamu Tanzania.

Mazungumzo yetu yalikuwa na ajenda kadhaa ikiwemo kumtambulisha Afisa Mtendaji Mkuu mpya wa Cosota, baada ya aliyekuwepo kumaliza muda wake.