Jan 30, 2013

Kwa hili la Idara ya Utamaduni, tasnia hii itaendelea kuyumba


Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo,
Dk. Fenela Mukangara

SERIKALI imekuwa ikijinadi kuwa inawajali wasanii ndiyo maana imeamua kuutambua mchango wao kwa kuirasimisha tasnia ya burudani - hasa filamu na muziki – ili wasanii wafaidi jasho la kazi yao, na imekuwa ikionesha kwa vitendo kuwa karibu na wasanii pindi kunapotokea msiba wa msanii maarufu, ingawa bado kuna maswali kadhaa ambayo yanajitokeza na kuleta maswali makubwa zaidi kama kweli inawajali.

Inashangaza kuona kuwa Wasanii ambao Serikali inajigamba kuwajali hadi leo tunapojigamba kuingia kwenye urasimishaji bado hawana sera (ya filamu kwa waigizaji au ya muziki kwa wanamuziki) inayowaongoza katika kufikia mafanikio ya tasnia yao. Pia inashangaza kuona kuwa Idara muhimu ambayo ndiyo uti wa mgongo wa sanaa nchini, ya Utamaduni limekuwa tatizo jingine kubwa kwa mustakabali wa maendeleo ya sanaa nchini.

Jan 23, 2013

Kwanini tuendelee kufuata nyayo badala ya kuongoza?


Ousmane Sembène, gwiji wa filamu barani Afrika

MAMBO ni tofauti kabisa, kile kinachotokea Nigeria ni tofauti na kile kinachotokea Afrika Kusini, Tasnia ya filamu ya Misri inaonekana kuwa na kiwango cha mbali mno ukilinganisha na ile ya Kenya, na nikijaribu kufupisha mambo, ni kweli soko la filamu barani Afrika ni soko tata kidogo. 

Nchini Nigeria, nadhani kilichoanza kutokea kinaweza kuwa mfano kwa hali ya soko hapo baadaye: Nollywood ilianza kama aina fulani hivi ya watu mfano wa wazimu/mhemko wa video za bajeti ndogo, zilizotengenezwa na wafanyabiashara zaidi kuliko watengenezaji wa filamu, na baadaye soko la ushindani likaanza kudai ubora na ndipo tulipoweza kuona filamu nzuri sana zilizokuja kuibuka baadaye kama ile ya Kunle Afolayan ya ‘The Figurine’.

Jan 16, 2013

Mkutano kati ya kamati ya serikali ya urasimishaji wa tasnia za filamu na muziki, wasambazaji na wazalishaji wa bidhaa za sanaa – Peacock Hotel, Januari 14, 2013



Dk. Vicensia Shule, akitoa dukuduku lake kuhusiana na changamoto za urasimishaji


Mkutano huo ulikuwa na ajenda zifuatazo:

i.                    Kufungua mkutano
ii.                  Kutoa muhtasari wa madhumuni ya serikali na hatua zilizofikiwa hadi sasa
iii.                Kuelezea hatua za upatikanaji wa stempu za kodi
iv.                Kupata taarifa ya hali halisi ya upatikanaji wa mashine za kubandika stempu
v.                  Kuzungumzia mikataba kati ya wafanyabiashara na wasanii
vi.                 Kupata maoni ya wazalishaji na kujua tofauti kati ya bidhaa zafilamuna bidhaa za muziki

Jan 3, 2013

Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo yatuma rambirambi msiba wa Sajuki


Sadiki Juma Kilowoko (Sajuki) enzi za uhai wake

Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara, amewatumia salamu za rambirambi, ndugu, jamaa na wasanii wote nchini kufuatia kifo cha msanii Juma Kilowoko (Sajuki) kilichotokea usiku wa kuamkia tarehe 02/01/2013 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Taarifa iliyotolewa leo, jijini Dar es salaam, Wizara ya Habari, Vijana na Utamauni na Michezo imepokea kwa masikitiko na huzuni kubwa taarifa za kifo cha msanii huyo na kuongeza kuwa kifo hicho ni pigo katika tasnia ya filamu hapa nchini.

Jan 2, 2013

Kwanini hatujifunzi kutoka Sekta ya filamu ya Afrika Kusini?


Moja ya kazi nzuri zilizotengenezwa Afrika Kusini

SEKTA ya filamu ya Afrika Kusini ni mahiri, inayokua na kuzidisha ushindani katika anga za kimataifa. Watengenezaji wa filamu wa ndani na wa nje wanatumia fursa mbalimbali zilizopo, maeneo ya kipekee - na gharama nafuu za uzalishaji na kiwango kizuri cha pesa ya Afrika Kusini dhidi ya dola ya Kimarekani, ambacho hufanya kuwepo unafuu wa hadi asilimia 40 katika kutengeneza filamu Afrika Kusini kuliko Ulaya au Marekani na unafuu wa hadi asilimia 20 zaidi kuliko Australia.

Kifo cha Sajuki chaacha simanzi nzito


Sajuki, enzi za uhai wake

Watu wengi wamepokea taarifa ya kifo cha Msanii maarufu wa filamu nchini Tanzania Sadiki Juma Kilowoko au Sajuki kama ambavyo anajulikana na wengi aliyefariki dunia alfajiri ya kuamkia leo katika hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salam alikokuwa akitibiwa.

Sajuki anajulikana na wengi kwa sinema zake za kashkash alikuwa akiugua maradhi ya muda mrefu mpaka kufikia hatua ya kupelekwa India kwa matibabu zaidi.