Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo,
Dk. Fenela Mukangara
SERIKALI imekuwa ikijinadi
kuwa inawajali wasanii ndiyo maana imeamua kuutambua mchango wao kwa
kuirasimisha tasnia ya burudani - hasa filamu na muziki – ili wasanii wafaidi
jasho la kazi yao, na imekuwa ikionesha kwa vitendo kuwa karibu na wasanii
pindi kunapotokea msiba wa msanii maarufu, ingawa bado kuna maswali kadhaa
ambayo yanajitokeza na kuleta maswali makubwa zaidi kama kweli inawajali.
Inashangaza kuona kuwa Wasanii
ambao Serikali inajigamba kuwajali hadi leo tunapojigamba kuingia kwenye
urasimishaji bado hawana sera (ya filamu kwa waigizaji au ya muziki kwa
wanamuziki) inayowaongoza katika kufikia mafanikio ya tasnia yao . Pia inashangaza kuona kuwa Idara muhimu
ambayo ndiyo uti wa mgongo wa sanaa nchini, ya Utamaduni limekuwa tatizo
jingine kubwa kwa mustakabali wa maendeleo ya sanaa nchini.