Wasanii wakifuatilia semina ya TRA kwenye ukumbi wa maonesho wa Makumbusho ya Taifa, Jumanne wiki hii
Pia nilikuwepo kwenye semina hiyo, hapa nipo na mdau
NIMEKUWA nikisisitiza kuwa
hakuna 'excuse' yoyote kwa wasanii katika kukuza pato lao, kuondokana na
umaskini na hata kushindana kimataifa kama
hawataingizwa kwenye mfumo rasmi ambao utawafanya watambulike ndani na nje ya
nchi ili kujenga mazingira ya wao kuweza kukopesheka, kupata fursa za kikazi na
kukuza kazi wanazozifanya. Katika mataifa mengine wasanii wako rasmi na
wameweza kuvuma na kupaa kiuchumi.
Lakini pia nimekuwa nikitoa
wito kwa serikali kutumia fursa ya kuirasimisha tasnia ya burudani hususani
filamu kwa kutuanzishia chombo cha kusaidia maendeleo ya miradi kama sehemu muhimu ya kuifanya sekta hii ifikie
tunapopataka, na ni msingi muhimu ambapo mkakati wowote wa utengenezaji wa
filamu unapaswa kujengwa.