Nov 27, 2012

Ni wiki ya majonzi kwa wasanii na wadau wa filamu nchini


 Mlopelo enzi za uhai wake

Wiki iliyopita ilishuhudia msanii aliyepata umaarufu mkubwa enzi za Kaole ya ITV, maaruf kwa jina la Mlopelo aliyefariki dunia mchana wa Alhamisi kwenye hospitali ya Temeke, jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa msemaji wa familia aliyejitambulisha kwa jina moja la Azizi aliyesema kwamba katika maisha yake yote, Mlopelo alikuwa anasumbuliwa na maumivu ya mwili yaliyokuwa yakitulia na kuibuka tena hadi umauti ulipomfika.