Katibu Mtendaji wa Bodi ya Ukaguzi wa Filamu, Joyce Fisoo
Katibu Mtendaji wa Basata, Ghonche Materego
WIKI iliyopita niliandika makala kuhusu umoja mpya wa wasanii, watayarishaji na wadau wa filamu ulioanzishwa hivi karibuni kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Leaders Club na kuweka historia mpya kwa kuifanya tasnia ya filamu kuzaliwa upya kwa kuwa na kundi moja lenye nguvu na uhamasishaji katika kutafuta maendeleo na pia kupambana na uharamia ambao umekuwa ukiwarudisha nyuma wasanii na kuwanufaisha wachache bila ya wao kutokwa jasho hata kidogo.