* MFDI-Tanzania wameanza rasmi mkakati wa mafunzo
Waziri wa Habari, Utamaduni Michezo na Vijana,
Emmanuel John Nchimbi
WIKI iliyopita, kuanzia Jumanne ya tarehe 22 Novemba hadi Jumamosi ya tarehe 26 Novemba, kulikuwa na warsha ya siku tano ambayo ni ya kwanza katika mkakati maalum uliowekwa na taasisi ya Media for Development International – Tanzania (MFDI-Tanzania), kuhakikisha kuwa tasnia ya filamu nchini “Swahiliwood” kama ambavyo wanapenda ijulikane, inafikia kile ambacho tasnia zingine duniani zimeweza, kwa kuandaa warsha iliyohudhuriwa na washiriki 25, wakiwemo watayarishaji wa filamu maarufu na waandishi maarufu wa script.
Warsha hii iliyoandaliwa na MFDI-Tanzania, ambayo mimi nilikuwa mmoja kati ya washiriki waliohudhuria mafunzo maalum ya jinsi ya utafiti na uandishi wa miswada andishi.