Oct 26, 2011

Tusipodhibiti sasa kazi chafu tujue kuwa tunaandaa bomu

 Kazi za utengenezaji sinema kama hizi zinahitaji nidhamu 
na maadili ya taaluma kama ilivyo kwa taaluma nyingine.

TAKRIBANI mwezi mmoja tu kuanzia sasa, nchi yetu itasherehekea miaka hamsini tangu tujipatie uhuru kutoka kwa wakoloni wa Kiingereza. Baada ya uhuru wa Tanganyika serikali katika kuthamini sanaa na utamaduni ilianzisha Wizara ya Utamaduni wa Taifa na Vijana iliyoundwa mwaka 1962, na rais wa Tanganyika na baadaye Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, alitamka wazi kuwa Utamaduni ndiyo kiini na roho ya Taifa.

Katika jitihada zake, nchi yetu ilipata kusifiwa sana kwa jitihada hizo za kushughulikia ukuzaji wa utamaduni katika duru nyingi za kimataifa. Hata hivyo, wakati tukiwa tunajiandaa kusherehekea miaka hii hamsini tangu uhuru, hali ilivyo sasa inatisha na kama hatua za dhati hazitachukuliwa, kazi iliyofanywa miaka ya nyuma, hasa mara baada ya uhuru na miaka takriban 20 iliyofuata, itapotea na tutajikuta tukiwa taifa lisilo na utamaduni wake.

Oct 19, 2011

Filamu zetu na athari zake katika jamii

 Waziri wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo
Dk. Emmanuel John Nchimbi

TUKIWA tunaelekea kutimiza miaka 50 tangu tuwe huru, jamii ya Kitanzania imeendelea kupoteza mila na tamaduni zake kila kukicha. Baada ya uhuru wa Tanganyika mwaka 1961, Wizara ya Utamaduni wa Taifa na Vijana iliundwa mwaka 1962, rais wa wakati huo, Mwalimu Julius Nyerere, alitamka wazi kuwa Utamaduni ndiyo kiini na roho ya Taifa, na nchi inayokosa utamaduni wake ni sawa na mkusanyiko wa watu usiokuwa na roho na hivyo kukosa sifa ya kuitwa taifa kamili.

Nalazimika kusema kuwa miaka hii hamsini ya uhuru nchi yetu inashuhudia mmomonyoko mkubwa wa maadili katika jamii huku tasnia ya sanaa/utamaduni ikionekana kutelekezwa kabisa na serikali yetu bila kujali kuwa tasnia hii imesheheni utajiri mkubwa ambao kama ungetiliwa maanani ungeliingizia taifa hili pato kubwa.

Oct 12, 2011

Filamu yaweza kukufanya uishi hata baada ya kifo!

 Susan Lewis (Natasha)

 Marehemu Dalillah Kisinda (Tabia)

 Wakati wa upigaji picha ya Naomi

FILAMU (Movie au Motion pictures) maana yake ni mfululizo wa picha zinazoonesha mwendo wa watu au vitu na kuonekana mbele ya watazamaji kupitia kioo cha seti ya televisheni (screen). Ni aina ya mawasiliano yanayotumiwa kwa ajili ya kuhadithia/ kusimulia au kuwaelezea watu kuhusiana na kujifunza fikra au mitazamo mipya katika jamii.

Watu tofauti katika kila pembe ya dunia huwa wanaangalia filamu ambazo zinasimulia hadithi fulani ikiwa kama kiburudisho, mafunzo au njia mojawapo ya upenzi.

Oct 7, 2011

Ubinafsi huu wa nini kwenye biashara ya filamu?

Kazi ya kurekodi filamu ikiendelea

Anti Ezekiel, mmoja wa wasanii wanaotingisha 
katika soko la filamu nchini

WAKATI tasnia ya filamu nchini ikiendelea kukua, imefahamika kuwa thamani ya kazi za sanaa (filamu) inaendelea kushuka siku hadi siku kutokana na sababu nitakazozieleza baadaye na kusababisha zitengenezwe filamu nyingi zisizo na ubora. Pia kumekuwa hakuna tafiti zinazofanywa kwa maana ya kuweka kumbukumbu (data) zinazowekwa kutusaidia katika kutambua thamani halisi ya tasnia na soko la filamu nchini.

Wadau wengi wa filamu wamekuwa wakiilalamikia serikali kuhusu kutoitilia maanani tasnia hii ambayo ingeweza kuwa suluhisho kubwa la ajira kwa vijana wengi, chanzo cha mapato ya nchi na ambayo ingesaidia kutangaza vivutio vya nchi na hivyo kuvutia watalii wengi na kuliingizia taifa pesa nyingi kupitia utalii.