Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Cyril Chami
Kuanzia mwaka 2006 kumekuweko na mchakato uliokuwa unaratibiwa na Rulu Arts Promoters, wa marekebisho ya sheria ya hakimiliki iliyoko ili kuondoa mapungufu yaliyopo. Kinachokwamisha sheria hii kwenda Bungeni ni Wizara husika - ya Viwanda na Biashara kuwa na kigugumizi. Hatimaye Waziri wa Viwanda na Biashara ametamka rasmi kuwa sasa wameondoa kigugumizi hicho:
Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko imethibitisha hayo kuwa iko katika mchakato wa kukamilisha muswada wa mabadiliko ya sheria ya hakimiliki na hakishiriki ili kudhibiti wizi wa kazi za wasanii nchini.