May 30, 2011

Wizara kukamilisha muswada wa hatimiliki na hakishiriki

 Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Cyril Chami

Kuanzia mwaka 2006 kumekuweko na mchakato uliokuwa unaratibiwa na Rulu Arts Promoters, wa marekebisho ya sheria ya hakimiliki iliyoko ili kuondoa mapungufu yaliyopo. Kinachokwamisha sheria hii kwenda Bungeni ni Wizara husika - ya Viwanda na Biashara kuwa na kigugumizi. Hatimaye Waziri wa Viwanda na Biashara ametamka rasmi kuwa sasa wameondoa kigugumizi hicho:

Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko imethibitisha hayo kuwa iko katika mchakato wa kukamilisha muswada wa mabadiliko ya sheria ya hakimiliki na hakishiriki ili kudhibiti wizi wa kazi za wasanii nchini.

May 25, 2011

Bodi ya Filamu: Wasaidieni wasanii

 Joyce Fissoo

Charles Kayoka

 Ukumbi maarufu wa Nkrumah wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam

BODI ya Ukaguzi wa Filamu Tanzania imewataka watalaam wa tasnia hiyo kusaidia wasanii kuhakikisha wanaandaa kazi nzuri zinazokidhi viwango vinavyokubalika Kitaifa na Kimataifa.

Kauli hiyo ilitolewa jijini Dar es salaam tarehe 18 Mei, mwaka huu na Katibu wa Bodi ya Ukaguzi wa Filamu Tanzania, Joyce Fissoo alipokutana na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wanaosoma Shahada ya Uzamili katika tasnia ya sanaa za Maonesho na Sanaa za Ufundi.

May 18, 2011

Ni kweli ustaa Tanzania haupatikani bila skendo?

 Mojawapo ya skendo zilizotamba kwenye magazeti

Vichwa vya habari kwenye magazeti vilivyojaa skendo chafu za wasanii wa filamu wa Tanzania

SEKTA ya filamu katika nchi yoyote ile ni sekta yenye nguvu sana, ikizingatiwa kuwa ina uwezo wa kuchangia kwa kiasi kikubwa mno katika uchumi wowote. Sekta hii ina uwezo mkubwa sana wa kuwa kichocheo cha ukuaji wa maendeleo ya haraka na ya kweli ya taifa ya nchi yoyote kwa kuzingatia utamaduni na saikolojia kwa maendeleo halisi na endelevu.

Ingawa sekta ya filamu ni moja tu kati ya sekta nyingi ndani ya tasnia ya burudani inayosimamia ubunifu, lakini filamu zinaaminika kuwa zina uwezo mkubwa sana wa kushawishi ama kutumika kwa ajili ya kuelimisha au kupotosha mambo katika jamii yoyote.

May 11, 2011

Tasnia ya filamu Tanzania bado ni sekta ya 'kuganga njaa'

Wasanii wa maigizo kama hawa wa kundi la ABY la Buguruni Malapa wanahitaji kuwezeshwa ili kufikia malengo yao


FILAMU kama zitachukuliwa kwa umakini mkubwa zinaweza kuwa chanzo kikubwa na muhimu sana katika kujenga taifa na zinaweza kutumika kama jukwaa la kuchochea mijadala nchini kote, lakini bahati mbaya bado tasnia hii hapa nchini imekuwa inakabiliwa na changamoto kadhaa.

Tasnia hii imekuwa ni sekta ya kujikimu, licha ya ukuaji wa haraka unaoonekana. Ukweli ni kwamba bado mavuno halisi ya tasnia hii katika kukuza pato la Taifa na hata watayarishaji walio wengi bado hawajafanikiwa kupata matokeo mazuri kiuchumi kupitia filamu.

May 4, 2011

Changamoto zinazoikumba tasnia ya filamu Tanzania

 Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Magolyo Maige

 Steven Kanumba katika movie ya This Is IT

INASEMWA kwamba eti tasnia ya filamu nchini Tanzania inazidi kukua siku hadi siku, kwani mtayarishaji wa filamu wa Tanzania anaishije leo ukitofautisha na miaka ya nyuma? Ni nani anayetoa fedha kuimarisha tasnia hii? Kama kweli tasnia imekua mbona hali halisi ya soko la filamu inabana sana uwezekano wa kuibuka kwa wasanii, watayarishaji au waongozaji wapya?...

Naamini kuwa filamu za kibongo zinakubalika sana katika ukanda wa Afrika Mashariki na maeneo ya ukanda wa Maziwa Makuu, lakini vipi kuhusu maisha ya wasanii wa Tanzania, je, wanapata stahili yao na wanaishi kwa kutegemea filamu pekee? Naomba majibu yako tafadhali”.

HAMMIE RAJAB: Gwiji wa filamu na simulizi aliyetabiri kifo chake

 Marehemu Hammie Rajab akitoa maelekezo kwa baadhi ya wasaniii wakati wa utengenezaji wa filamu ya simu ya Kifo mjini Tabora

SAID K. RAJAB
Dar es Salaam

NINA 'projects' nyingi bado sijamaliza... sasa nimeanza kuandika 'script' ya kitabu changu, Ama Zao Ama Zangu. Nataka iwe filamu. Mwenyezi Mungu akiniweka hai, InshaAllah, itakuwa moja ya filamu bomba sana!”

Ni maneno ya mwisho kabisa ambayo Hammie Rajab aliniambia, wakati nilipokwenda kumuona nyumbani kwake, Magomeni Mwembechai, siku tatu kabla hajafariki dunia. Alikuwa amelala kitandani, akiwa na maumivu makali sana ya tumbo.