Apr 27, 2011

Tutumie watunzi wazuri wa stori kuboresha filamu zetu

 Marehemu Hammie Rajab

 Marehemu Hammie Rajab akiongoza upigaji picha za filamu

ALHAMISI ya Aprili 21, 2011 saa tatu asubuhi, nilipokea ujumbe mfupi kwenye simu yangu uliotoka kwa Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania, Simon Mwakifwamba, akinijulisha kuhusu kifo cha mmoja wa watunzi mahiri wa vitabu na muongozaji wa filamu nchini ambaye nchi hii imepata kumshuhudia, Hammie Rajab.

Mwakifwamba alinijulisha kuhusu msiba huo ambao umeacha pigo sio tu kwa wapenzi wa riwaya bali kwa tasnia nzima ya filamu nchini.

Ramsey atoa somo kwa waigizaji filamu bongo

 Ramsey Noah katika pozi

Wasanii wa Tanzania wakiwa na muigizaji kutoka Nigeria, 
Ramsey Noah.

MSANII maarufu wa Nollywood, Ramsey Noah Atashirikiana na muigizaji maarufu wa filamu nchini, Steven Kanumba katika filamu ya Devil's Kingdom. Ramsey ambaye yupo jijini, atashiriki katika filamu hiyo ambayo imeandaliwa na Kanumba na kwa sasa iko hatua za mwishoni za maandalizi.

Akizungumza na waandishi wa habari jana katika mkutano uliofanyika hoteli ya Peacock jijini, Ramsey alisema amefurahishwa kushirikishwa kucheza filamu hiyo na Kanumba kwani anaamini ushiriki wake utakuwa chachu na changamoto kwa wasanii wa hapa nchini.
“Nimefurahi sana, hii itakuwa ni mara ya pili kushiriki na Kanumba kucheza filamu na kwa kufanya hivi kama Waafrika tunapanua wigo wa ubora wa kazi kwani kila mmoja anajifunza kutoka kwa mwenzake.

Apr 20, 2011

Wasanii kukubali kutumiwa kisiasa ni kujimaliza wenyewe

 Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF), 
Simon Mwakifwamba

 Msanii maarufu na Mbunge wa jimbo la Mbeya Mjini,
Joseph Mbilinyi maarufu kwa jina la Sugu

HISTORIA huwa haina haja na wale wote wenye kushindwa, labda tu kunukuu tarehe walizokutwa na umauti wao... na hii kidesturi huwa ni katika kila fani.” Ni msemo nilioufahamu miaka mingi iliyopita, na ninaamini una maana kubwa mno kwa yeyote anayejiita mwanaharakati.

Tasnia ya filamu hapa Tanzania ilikuwa ikipiga hatua siku hadi siku, lakini kwa siku za karibuni imeonekana kudorora. Kiukweli sanaa hii ipo chumba cha wagonjwa mahututi ikisubiri kupelekwa mochwari hasa kwa hiki kinachojitokeza sasa ambacho kwangu ni kama mazingaombwe.

Apr 13, 2011

Tatizo kubwa kwenye filamu zetu ni kukosa waongozaji

 Quentin Tarantino, mmoja wa waongozaji filamu 
wa Hollywood wanaoheshimika duniani

 Steven Kanumba, mmoja wa waongozaji filamu Tanzania

WIKI iliyopita msomaji mmoja wa makala zangu alinitumia ujumbe kupitia baruapepe akitaka kujua mtazamo wangu kuhusu mapungufu yaliyopo katika filamu za Kibongo, huku yeye akitupia lawama moja kwa moja kwa waigizaji na waandishi wa muswaada andishi (scriptwriters) kwa kutokuwa na uwezo.

Msomaji huyo aliyejitambulisha kwa jina la Masengwa, mkazi wa Kazima, Tabora alisema kuwa waigizaji wengi wa filamu za Kibongo wamekuwa wanashindwa kabisa kuuvaa uhalisia wanapoigiza! Akitolea mfano wa filamu moja (anaitaja jina) ambapo ilionekana mwigizaji akiigiza analia lakini uso wake ulikuwa umebeba tabasamu la chati!

Apr 11, 2011

Athari ya filamu za Magharibi katika nchi zinazoendelea

 Original Sin, mojawapo ya filamu maarufu za Kimagharibi zinazoathiri utamaduni wetu

TAFSIRI ya filamu ni mfululizo wa picha zinazoonesha mwendo wa watu au vitu na kuonekana mbele ya watazamaji kwenye skrini. Ni aina ya mawasiliano yanayotumiwa kutolea hadithi au kuwafundisha watu kuhusiana na fikra au mitazamo mipya katika jamii. Wafuatiliaji wa filamu huangalia filamu ambazo zinaelezea hadithi fulani kama njia mojawapo ya kuburudika, kujifunza au kwa sababu ya upenzi tu.

Filamu zilizoibuka kuanzia karne ya kumi na tisa, zimekuwa kishawishi kikubwa na mawasiliano ghali katika karne hii ya ishirini na moja. Hadi sasa hakuna aina nyingine yoyote ya sanaa ambayo imesambaa kwa ufanisi mkubwa na kuvuka mipaka ya kiutamaduni katika mataifa mengi kama ilivyo kwa filamu.