Mar 30, 2011

Ukuaji wa Tasnia ya Filamu ni Chachu Katika Kukuza Ajira

 Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Harry Kitilya

TAKRIBAN miezi miwili iliyopita nilibahatika kukutana na kiongozi mmoja mwandamizi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), katika kikao kisicho rasmi wakati akijaribu kuangalia uwezekano wa kukusanya mapato kupitia tasnia ya burudani, hasa muziki na filamu.

Japo mimi si kiongozi wa taasisi yoyote lakini nilipata heshima ya kukutanishwa naye kwa kuwa wanathamini mchango wangu katika kuikuza na kuiendeleza tasnia hii. Katika makala hii sitaelezea tulichozungumza, nitajaribu kuongelea jambo moja ambalo nadhani ni kikwazo kinachoikabili Mamlaka ya Mapato katika kukusanya mapato kupitia tasnia ya burudani.

Mar 23, 2011

Bodi ya Ukaguzi wa Filamu inafanya nini kuinusuru tasnia ya filamu?

Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo George Mkuchika 
katika picha ya pamoja na viongozi wa Bodi ya Ukaguzi wa Filamu mara baada ya uzinduzi. Kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Bodi hiyo Bi. Rose Sayore.

 Msanii Hisani Muya maarufu kwa jina la Tino 
aliyecheza filamu ya Shoga iliyoleta tafrani

MAJUZI jamaa zangu ambao ni watayarishaji wa filamu za Kibongo walinikumbusha jambo la msingi sana ambalo nahisi napaswa kuliandikia makala, jambo ambalo kwa mtu asiyefahamu anaweza awashangae sana hasa pale walipoonekana kutoijua kabisa Bodi ya Ukaguzi wa Filamu na Michezo ya Kuigiza.

Lakini si wao tu bali watayarishaji na wasanii wengi niliowahi kukutana nao hawaijui, si kwa makusudi bali ndiyo hali halisi ilivyoachwa iwe.

Mar 16, 2011

Wasanii kuisusa Cosota ni kujimaliza wenyewe

*Cosota ni ya wanachama, si taasisi ya Serikali kama wanavyodhani
*Wanachama wa Cosota wana nguvu ya kisheria kuwashughulikia wezi

Katibu Mtendaji wa Cosota, Yustus Mkinga

NI jambo la kufurahisha sana kuona tasnia ya filamu Tanzania (Bongo movies), inazidi kushamiri na kukubalika ndani na nje ya mipaka yetu.

Licha ya mafanikio hayo, bado zipo changamoto nyingi zinazowakabili wasanii wa filamu pamoja na filamu zao kupendwa na kusambaa sehemu nyingi duniani. Mambo yanayowakwaza watayarishaji na wasanii wengi wa filamu ni kutokuzijua haki zao na wala hakuna jitihada zozote zinazofanywa kutaka kuzijua.

Mar 9, 2011

Elimu, ubinafsi na kukosa malengo vinaikwaza tasnia ya filamu nchini

Kupata mafunzo ni jambo muhimu, picha hii inaonesha 
baadhi ya washiriki wa mafunzo ya utengenezaji filamu 
katika Kituo cha Utamaduni cha Ujerumani (Goethe Institut) 
yaliyofanyika mwaka jana

IJUMAA iliyopita nilikutana na muongozaji na mwandishi wa miongozo ya filamu (script), James Gayo, ambaye pia ni msomaji wa makala zangu na tulipata nafasi ya kubadilishana mawazo kuhusu yanayojiri katika tasnia ya filamu hapa nchini.

Gayo hakusita kunieleza wasiwasi wake kuwa pamoja na ujuzi alionao kuhusu filamu lakini amekuwa akisita sana kuingia katika utengenezaji wa filamu za kibiashara kwa soko la filamu nchini kwa sababu ya matatizo yanayoathiri sekta ya filamu ambayo hadi sasa hakuna juhudi zozote zinazochukuliwa kuyatatua. Matatizo hayo ni kutokuwepo malengo, mipango mibovu na uchoyo usiokuwa wa lazima.

Mar 2, 2011

Tutafakari kabla ya kusema au kutenda, ili kudumisha maadili

 Anti Ezekiel na Steven Kanumba katika moja ya filamu walizoigiza

 Flora Mvungi, mmoja wa waigizaji maarufu wa kike

MAKALA yangu ya wiki iliyopita; Utamaduni wa Mtanzania ni upi...” imeibua mjadala nisioutarajia kutoka kwa wasomaji wa makala yangu, mjadala uliopelekea baadhi yao kusema kuwa makala yangu haikuwa wazi sana kuhusu suala la filamu ya shoga huku wakiwa hawajui nini msimamo wangu kuhusu filamu hiyo, na wengine wakielekeza lawama zao kwenye Bodi ya Ukaguzi wa Filamu na Michezo ya Kuigiza kuwa haifanyi kazi zake ipasavyo.

Si nia ya makala hii kuendeleza malumbano na kumtupia lawama mtu au taasisi fulani, lakini nadhani nina wajibu kukemea au kuelekeza yalipo mapungufu, na ninaamini kuwa yapo mambo kadha wa kadha ambayo yanahitaji mjadala wa kina ili tupate ufumbuzi kuhusu kile kinacholalamikiwa na jamii kuhusu sanaa yetu.