Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Harry Kitilya
TAKRIBAN miezi miwili iliyopita nilibahatika kukutana na kiongozi mmoja mwandamizi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), katika kikao kisicho rasmi wakati akijaribu kuangalia uwezekano wa kukusanya mapato kupitia tasnia ya burudani, hasa muziki na filamu.
Japo mimi si kiongozi wa taasisi yoyote lakini nilipata heshima ya kukutanishwa naye kwa kuwa wanathamini mchango wangu katika kuikuza na kuiendeleza tasnia hii. Katika makala hii sitaelezea tulichozungumza, nitajaribu kuongelea jambo moja ambalo nadhani ni kikwazo kinachoikabili Mamlaka ya Mapato katika kukusanya mapato kupitia tasnia ya burudani.