Feb 25, 2011

Kwaheri Tabia wa Kidedea

 
Tabia alipokuwa akiigiza katika filamu ya Usiku wa Taabu
 Tabia alipokuwa akiigiza katika filamu ya Naomi

HAMISI KIBARI
Dar es Salaam

CHRIS Magori, mwandishi wa miongozo ya filamu (script), mtunzi na muongozaji (director), aliipenda hadithi niliyowahi kuiandika katika gazeti la Nipashe miaka ya nyuma ikiitwa 'Usiku wa Taabu'. Aliipenda hadithi hiyo kwa maana ya kuifanya filamu. Wakati huo, mwaka 2004, tasnia ya filamu ilikuwa inazidi kushika kasi nchini mwetu, lakini si kwa kiwango cha sasa.

Katika hadithi hiyo niliyoiandika kutokana na kisa cha kweli, mhusika mkuu ambaye ni mke wa mchungaji, alikuwa na tabia isiyoendana kabisa na hadhi yake. Kwa lugha nyingine alikuwa mhuni ambaye alidiriki kwenda gesti na wanaume hususan mumewe anapokuwa katika safari za kichungaji.

Feb 23, 2011

Utamaduni wa Mtanzania ni upi, na unahusishwaje na filamu zetu?

 Filamu iliyozua utata ya Shoga

 Filamu ya Off Side

KWA kweli suala la mila na utamaduni wa Mtanzania linatatiza sana. Tunaposema utamaduni na mila za Watanzania hasa tunamaanisha nini kwa Tanzania yenye zaidi ya makabila 120 ambayo kila moja lina mila na utamaduni wake? Huu utamaduni na mila za Watanzania ni upi hasa?

Haya ni baadhi ya maswali ambayo kila mtetezi wa mila na utamaduni ndani ya jamii za Kitanzania anapaswa kuyajibu. Vinginevyo tutakuwa tukiimba wimbo tusioujua maana yake, na hii haitatusaidia kufikia malengo tunayoyapigania.

Feb 22, 2011

Wasanii watakiwa kuacha kulewa sifa

Sehemu ya mji wa Morogoro

Husna Posh (Dotnata), mmoja wa wasanii wenye mafaniko makubwa

Na Ashton Balaigwa
Morogoro

Wasanii nchini wametakiwa kuacha kulewa sifa mara baada ya kupata mafanikio na badala yake watumie vipaji walivyonavyo kuelimisha kwa kutumia njia zitakazoisaidia jamii kutambua mahala tulipo na tunakoelekea.

Wito huo umetolewa na mwanasheria wa Kituo cha Wasaidizi wa Sheria kwa Wanawake na Watoto cha mjini Morogoro, Aman Mwaipaja, wakati akizungumza na wasanii chipukizi wa maigizo wa Kikundi cha Mikano Arts Group.

Feb 21, 2011

Serikali yasitisha usambazaji wa filamu ya Shoga


 TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

 Poster ya filamu ya Shoga

Hisani Muya (Tino), mtunzi na mhusika mkuu wa filamu ya Shoga

Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo imeiagiza Kampuni ya kutengeneza filamu ya 'Al-Riyamy Production Company' kuwasilisha Filamu ya 'Shoga' kwa Bodi ya Taifa ya Ukaguzi wa Filamu kwa ajili ya ukaguzi.

Aidha Kampuni hiyo pia imeagizwa kutoisambaza Filamu ya 'Shoga' na kusitisha hatua nyingine yoyote kuhusiana na filamu hiyo hadi hapo Bodi ya Taifa ya Ukaguzi wa Filamu itakapojiridhisha kuwa filamu hiyo inakidhi kuonyeshwa hadharani kama ilivyoainshwa katika Sheria ya Filamu na Michezo ya Jukwani Namba 4 ya mwaka 1976.

ARTERIAL Network: Mtandao wa wasanii uliozinduliwa Tanzania

 Waziri wa Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo wa Zanzibar, 
Abdillah Jihadi aliyekuwa mgeni rasmi siku ya uzindua 
wa Mtandao wa ARTERIAL Tanzania. Wengine ni 
Mwenyekiti mpya wa Mtandao huo nchini, Laurian Kipeja (kati) 
na kushoto ni mwakilishi wa Mtandao huo kwa Afrika, 
Telesphore Mbabizo.

Picha ya pamoja na Mgeni Rasmi.
Baadhi ya wajumbe waliohudhuria mkutano wa uzinduzi wa Mtandao wa ARTERIAL Tanzania

Mtandao wa wasanii Barani Afrika unaojulikana kwa jina la ARTERIAL Network, umezindua tawi lake nchini Tanzania na tayari umepata viongozi watakauongoza kwa kipindi cha miaka mwili. Uzinduzi wa mtandao huo ulifanywa na Waziri wa Habari, Utamaduni na Utalii wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) Mh. Abdillahi Jihadi, katika hoteli ya Zanzibar Grand Palace.

Feb 17, 2011

Shirikisho la Filamu Tanzania laitaka serikali kuwekeza kwenye filamu



Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) limeitaka serikali kuwekeza katika kazi za sanaa ya muziki na filamu ili kukuza pato la taifa. Hayo yalisemwa na Rais wa sirikisho hilo, Simon Mwakifwamba, katika uzinduzi rasmi wa shirikisho hilo ulioambatana na Tamasha la Filamu za Kitanzania “The Mwalimu Nyerere Film Festival” lililoanza Februari 14 katika viwanja vya Leadres Club vilivyopo Kinondoni, jijini Dar es Salaam.

Wahujumu wa kazi za Wasanii waanikwa mkoani Pwani

 Kazi feki za sanaa zikiwa tayari kwa kuuzwa

Kazi feki zikitayarishwa kuchomwa huko China

Kundi la watu ambao wamekuwa wakihujumu kazi za wasanii mbalimbali nchini limebainika mkoani Pwani. Uchunguzi uliofanywa kwa muda mrefu katika magulio kadhaa ya mkoa wa Pwani umebaini kuwapo kwa kundi kubwa la wafanyabiashara wanaouza kazi za Wasanii mbalimbali zilizodurufiwa (duplicated) kwa bei ya chini na kusababisha wasanii kutofaidika na kazi zao.

Waziri Nchimbi, ni lini sekta ya filamu itakuwa rasmi?

 Waziri wa Habari, Maendeleo ya Vijana, 
Utamaduni na Michezo, Emmanuel Nchimbi

KWANZA kabisa napenda nikupongeze kwa kuteuliwa kuwa Waziri wa Habari Vijana na Michezo, nikitumaini kuwa Rais Jakaya Kikwete amekuona unafaa zaidi kuiongoza wizara hii nyeti inayohusu mustakabali wa utamaduni wa Watanzania.

Nakubaliana na wanaosema kuwa uteuzi wako kuiongoza wizara hii umewapa wanahabari na wasanii tumaini jipya kwa sababu tangu nchi yetu ipate uhuru miaka 49 iliyopita, wizara hiyo ilimpata waziri mmoja tu, Marehemu Ahmed Hassan Diria, aliyesimamia kwa dhati maendeleo ya wanahabari/ wasanii na ustawi wa tasnia nzima.

Feb 9, 2011

Kutoka Mahoka, Pwagu na Pwaguzi hadi maigizo yenye mizaha!

Marehemu Mzee Pwagu, mmoja wa wachekeshaji 
waliojizolea umaaruf mkubwa nchini

Said Ngamba (Mzee Small), mchekeshaji 
wa kwanza Tanzania kuigiza kwenye Televisheni

Charlie Chaplin, mchekeshaji maarufu wa enzi za 'silent film'

Mr Bean, mchekeshaji maaruf wa Uingereza

WIKI iliyopita nilimkuta binti yangu wa miaka 6, Magdalena, akiwa na mama yake wameketi sebuleni wakiangalia katuni za Tom & Jerry, nilichukua rimoti na kuwabadilishia nikiweka kipindi cha Komedi kinachorushwa na moja ya vituo vyetu vya televisheni, kipindi kilichokuwa gumzo sana siku za nyuma na kilipendwa na watu wa rika zote.

Niliweka kipindi hicho nikijua wao ni wafuatiliaji wakubwa, kuna wakati tulikuwa tukigombana kwa kuwa walitaka kuangalia komedi hata pale nilipokuwa nikifuatilia habari muhimu kwenye vituo vingine.

Feb 8, 2011

Steps na Pilipili Entertainment kwenda kimataifa

 Nembo ya filamu ya nchi za Caribbean

Nembo ya Tamasha la Filamu Zanzibar

Poster ya filamu ya Deception

Kampuni ya usambazaji wa filamu ya Steps Entertainment na ile ya utengenezaji filamu ya Pilipili Entertainment ziko mbioni kupata soko la kimataifa kutokana na filamu zao kunadiwa katika tamasha la kimataifa la Fair International Film Festival sambamba na Iran Film Market. Taarifa za kampuni hizi zimetolewa na Meneja wa Zanzibar International Film Festival (ZIFF), Daniel Nyalusi, kuwa Iran watatumia filamu za kampuni hizo kupata soko la kimataifa.

Kwa mujibu wa Ziff, wanajaribu kupata wasambazaji, wazaalishaji na wawekezaji wa filamu duniani, ambao wangependa kununua, kusambaza, kutengeneza au kufanya kazi ya pamoja na kiwanda cha filamu hapa nchini.

Feb 2, 2011

Pamoja na changamoto, soko la filamu litakua na kudumu

 Said wa Ngamba, mmoja wa waigizaji nguli
katika tasnia ya filamu Tanzania

 Baadhi ya waigizaji wakiwa kwenye kikao cha wadau wa filamu

* Wauzaji wa filamu wanapaswa kushirikiana na makampuni yenye mitandao nchi nzima
* Mafunzo juu ya maarifa pia yapewe kipaumbele

USIKU wa Jumatatu wiki hii sikupata usingizi kabisa, nilijiwa na mawazo yaliyoshindikana kufutika akilini mwangu, mawazo ambayo yameendelea kunitesa hadi niandikapo makala hii, kuwa kuna nguvu kubwa inayotambaa mikononi mwa wauzaji wa filamu nchini... Kubwa sana. Kitendo kinachofanywa na wauzaji kuwa na umuazi wa mwisho kama wauze kazi au la, na hakuna njia mbadala kinazidi kuwatesa watayarishaji wengi wa filamu hapa nchini.

Feb 1, 2011

Wasanii Tanzania wanatakiwa kujifunza Kiingereza

Christina Innocent "Mama Bishanga" (kushoto), 
na mwanae Hendrick Nambira "Kenny" (kulia), 
akizungumza na Waandishi wa Habari ambao 
hawapo kwenye picha, kwenye ukumbi wa 
Habari MAELEZO


 Wasanii maaruf wa sinema Tanzania, 
Vincent Kigosi (Ray) na Steven Kanumba

Emmanuel Myamba, mmoja wa waigizaji wa filamu nchini wanaoijua vizuri lugha ya Kiingereza

Wasanii wa sanaa za maonesho na filamu nchini wametakiwa kuongeza bidii kujifunza lugha ya Kiingereza ili waweze kupanua wigo wa soko la kazi zao kimataifa. Mwito huo ulitolewa jijini Dar es Salaam siku ya Jumatatu na msanii maaruf wa maigizo nchini, Christina Innocent maaruf kwa jina la Mama Bishanga, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu hali ya sanaa hapa nchini.

BASATA kuwakutanisha wasanii wa Tanzania na wa nje

 Katibu Mtendaji wa Basata, Gonche Materego

 Sehemu ya umati wa washiriki wa Jukwaa la Sanaa, Basata

Baraza la Sanaa la Taifa (Basata), linatarajia kuwakutanisha wasanii wa Tanzania na wasanii wa nje ili kubadilishana ujuzi na uzoefu utakaoitambulisha sanaa kwenye soko la kimataifa.

Akizungumza jijini Dar es Salaam kwenye Jukwaa la Sanaa Jumatatu wiki hii, Katibu Mtendaji wa Basata, Gonche Materego alisema kuwa, kuwakutanisha wasanii wa nchini na wale wa kutoka nje ya nchi hasa nchi jirani kutaweza kuleta mabadiliko makubwa katika tasnia ya sanaa.