Tabia alipokuwa akiigiza katika filamu ya Usiku wa Taabu
Tabia alipokuwa akiigiza katika filamu ya Naomi
HAMISI KIBARI
Dar es Salaam
CHRIS Magori, mwandishi wa miongozo ya filamu (script), mtunzi na muongozaji (director), aliipenda hadithi niliyowahi kuiandika katika gazeti la Nipashe miaka ya nyuma ikiitwa 'Usiku wa Taabu'. Aliipenda hadithi hiyo kwa maana ya kuifanya filamu. Wakati huo, mwaka 2004, tasnia ya filamu ilikuwa inazidi kushika kasi nchini mwetu, lakini si kwa kiwango cha sasa.
Katika hadithi hiyo niliyoiandika kutokana na kisa cha kweli, mhusika mkuu ambaye ni mke wa mchungaji, alikuwa na tabia isiyoendana kabisa na hadhi yake. Kwa lugha nyingine alikuwa mhuni ambaye alidiriki kwenda gesti na wanaume hususan mumewe anapokuwa katika safari za kichungaji.