Mwandishi wa makala haya, Bishop J. Hiluka
SIKU nilipopigiwa simu na mhariri wa gazeti hili akinitaka tuonane sikufikiria kabisa kama angenikabidhi jukumu la kuandika makala kwenye gazeti lake. Sikufikiria kwa sababu sikudhani kama angeweza kunifikiria mimi niandike badala ya wachambuzi wengi maarufu na wa muda mrefu waliopo ambao tayari wameshajijengea heshima kubwa katika uandishi.
Nilisita sana kukubali kwa kuwa sikudhani kama ningeweza kukidhi kiu ya wasomaji, lakini nilipokumbuka uzalendo wangu na kiu yangu ya kutaka tasnia ya filamu hapa Tanzania ikue nikakubali mara moja.