Mzee Rashid Mfaume Kawawa, mmoja wa Watanzania wa mwanzo kucheza na kuongoza filamu kwenye miaka ya 1950.
Serikali ya Kikoloni katika koloni la Tanganyika ilianzisha rasmi Kitengo cha Filamu cha Tanganyika mapema mwaka 1948. Ilipofika mwanzoni mwa miaka ya 1950, tayari kulikuwa na vitengo vya filamu vya kudumu katika Afrika Mashariki.
Tanganyika (sasa Tanzania) kitengo hicho kiliweza kutengeneza sinema kumi na sita (zote za miaka ya 1950) za ukulima wa pamba. Ni katika kipindi hicho ndipo mzee wetu, mzee Rashid Mfaume Kawawa alipopata kuwa mmoja kati ya waigizaji wa filamu wa mwanzo kabisa wa Kitanzania na kufungua njia kwa Watanzania wengine.