Oct 31, 2009

Kilivyoanzishwa Kitengo cha Filamu Tanganyika (Tanzania Bara)

Mzee Rashid Mfaume Kawawa, mmoja wa Watanzania wa mwanzo kucheza na kuongoza filamu kwenye miaka ya 1950.

Serikali ya Kikoloni katika koloni la Tanganyika ilianzisha rasmi Kitengo cha Filamu cha Tanganyika mapema mwaka 1948. Ilipofika mwanzoni mwa miaka ya 1950, tayari kulikuwa na vitengo vya filamu vya kudumu katika Afrika Mashariki. 

Tanganyika (sasa Tanzania) kitengo hicho kiliweza kutengeneza sinema kumi na sita (zote za miaka ya 1950) za ukulima wa pamba. Ni katika kipindi hicho ndipo mzee wetu, mzee Rashid Mfaume Kawawa alipopata kuwa mmoja kati ya waigizaji wa filamu wa mwanzo kabisa wa Kitanzania na kufungua njia kwa Watanzania wengine.

Oct 26, 2009

Ujio wa Sinema katika bara la Afrika

Waongozaji wa sinema za Kitanzania, Sulesh Marah na Bishop J. Hiluka

Nembo ya soko la Filamu nchini Nigeria

Ieleweke kuwa kwa miaka mingi tu Afrika imekuwa ikiwasilishwa katika uwanja wa filamu kama bara lenye giza na mataifa ya Ulaya na Magharibi. Matamanio ya kueneza propaganda katika kipindi cha vita kuu ndiko kulikosababisha na kuibuka upya kwa ari katika mataifa ya Magharibi, kwa mfano nchini Uingereza walitengeneza sinema kama “FORTY-NINTH PARALLEI (1941)”, “WENT THE DAY WELL? (1942)”, na “THE WAY AHEAD (1944)” zote zikiwa zina lengo lile lile la kueneza propaganda.

Historia ya Filamu Duniani

Historia ya sinema duniani inaanzia kwa Bw. William Kennedy Laurie Dickson aliyekuwa injinia mkuu wa Edison Laboratories ya Marekani. Huyu Dickson ndiye anayesadikiwa kuwa mvumbuzi na “baba wa filamu duniani”, alivumbua mfumo wa picha unaojulikana kitaalamu kama “Celluloid Strip”, yaani mkanda maalum uliokusanya picha za matukio mfuatano (sequence of images) yaliyopigwa kwa kamera (photographing) maalumu ya picha za matendo (moving images) na kuzionesha kwa njia ya sinema (projecting moving images).


Kinetograph

Oct 25, 2009

Umewahi kusikia juu ya KITI CHEUPE?

Florian L. Mtaremwa (Ray) akiwa kwenye ofisini zake katika studio ya RAV ProductionOfisi hiyo ipo eneo la Malapa, Ilala.

Florian Lawrence Mtaremwa (maarufu kama Ray wa Splendid), Mkurugenzi na mmiliki wa kampuni ya RAV Production ameamua kuja kivingine katika sanaa ya filamu ya Bongo baada ya kutunga na kuandaa sinema ya kusisimua inayoitwa 'White Chair' au Kiti Cheupe kwa Kiswahili. Sinema hiyo ni ya aina yake katika nchi hii ambayo unaweza kuifananisha na sinema kali za Hollywood kama vile Anaconda na nyingine za kusisimua ambazo zitakufanya usikae vizuri kwenye kiti chako pindi uziangaliapo.

Oct 24, 2009

Wadau wa Filamu wanapaswa kujiendeleza

Pichani ni wadau wa filamu Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kumaliza mafunzo ya Actors Directing yaliyokuwa yakitolewa kwenye Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Idara ya Sanaa na kuendeshwa na wataalam toka Ujerumani. Bishop J. Hiluka wa kwanza kulia kwa walioketi kwenye benchi (mwenye tshirt nyeupe na suruali ya jeans ya bluu). Anayemfuatia ni Matthias Luthard, mtaalam toka Ujerumani.

Oct 21, 2009

Mtazamo wa Wazungu kwa Waafrika

Wasanii Hemed Suleiman na Yusuf Embe wakipozi wakati wa upigaji picha ya Blackmail eneo la Sunrise Hotel, Kigamboni.


Waafrika katika filamu za Wazungu mara nyingi walikuwa wakifanywa waonekane (na bado wanaendelea kuonekana) ni washenzi, watu wa chini, wafungwa, nk. Wakati mwingine huwa wanafanywa waonekane wakatili sana na wanaoamini mambo ya kishirikina.

Nimeshawahi kuelezea kwenye makala zangu kuwa wakoloni  walianzisha mpango maalum hapa Afrika Mashariki uliojulikana kama “Bantu Education Experiment”. Nitajadili kwa kirefu siku nyingine kuhusu Bantu Education Experiment. 

Oct 16, 2009

John Lister aja na BLACKMAIL

John Lister kashika CAMERA, mbele ya Simon Mwapagata (Rado) katika pozi la kufa mtu. 


Picha kali ya Kiswahili itakayoingia sokoni wakati wowote kuanzia mwezi wa ujao (Novemba,2009) imeandaliwa na John Lister, imepigwa picha na Rashid Mrutu na kuongozwa na Bishop J. Hiluka. Inajulikana kwa jina la Blackmail. 

Oct 13, 2009

Hii ndo' sababu naipenda sana AFRIKA ...

Makazi ya Kiafrika
Kweli hii ndo' Afrika. Lazima tujivunie Uafrika wetu ati!

Bara la Afrika limejaaliwa mandhali za kuvutia na wananchi wake wakarimu. Ndiyo maana inasemwa kuwa "Afrika Hakuna Matata!" Kwa Waafrika kila kitu huja kwa wakati wake wala hakuna makuu. Kwa miaka mingi sana bara la Afrika limekuwa likichukuliwa kuwa ni bara la giza na mataifa ya Ulaya na Marekani. Lakini hiyo hainifanyi kutoipenda Afrika.

Mafanikio ya Sinema za Hollywood


Watengeneza filamu wa Kimarekani wakiwajibika.


Soko la filamu la Marekani au kama linavyojulikana na wengi ‘Hollywood’, jina linalotokana na eneo la kijiografia lililopo katikati ya California, limeweza kufikia nafasi lilipo sasa si kwa bahati tu, bali lilitokana na jitihada kubwa na mikakati ya dhati iliyofanywa kitaifa. Hollywood imefanikiwa kuzalisha na kusambaza sinema zake nchi zote hadi kufikia kulitawala soko la sinema duniani.

Kukua kwa Sekta ya Filamu Duniani





Matatizo na ukosefu wa ajira kwa vijana ndiyo yaliyowachochea vijana wengi kujitumbukiza kwenye Sekta ya Filamu, na hivyo kupelekea wengi wao hivi sasa katika mataifa mengi (ikiwemo Tanzania) wakijikuta wamepata mkombozi wa ajira kupitia filamu kama inavyoonekana kwenye picha hizi.

Oct 5, 2009

Je, unadhani wewe ni mwandishi mzuri wa skripti? SOMA HAPA...

Bishop J. Hiluka akiandaa script kwa ajili ya kutengenezwa sinema

"Like Father like Daughter..."
Magdalena Hiluka (4) pichani akijifunza kusoma. Si vibaya kuwafuatilia wanetu ili kujua vipaji walivyonavyo kwa ajili ya kuviendeleza.

Jifunze jinsi ya kuboresha uandishi wako ili kazi yako isomeke kama ambavyo msafiri asomavyo ramani.

Kila siku nimekuwa nikisisitiza kuwa sinema bora hupimwa kwa vigezo vitano; skripti nzuri, waigizaji wazuri, muongozaji mzuri, wapigapicha wazuri, na mhariri mzuri. Skripti ndiyo inayoibeba sinema, na endapo hutakuwa na skripti nzuri iliyotokana na hadithi nzuri basi ujue kuwa kazi nzima itakosa mwelekeo.

Oct 1, 2009

Sinema za Kizazi Kipya cha Tanzania

James Gayo, muongozaji filamu wa Tanzania. Hapa anaongoza upigaji picha wa sinema "The Trip", nje kidogo ya mji wa Kampala-Uganda.

Kuanzia miaka ya 1990 hadi sasa nchi yetu imeshuhudia ongezeko kubwa la utengenezaji na utoaji wa sinema (za kizazi kipya) kila kukicha hali ambayo inaambatana na uwepo wa malalamiko mengi kutoka kwa viongozi, wasomi na wadau wa sekta ya filamu kuwa sinema nyingi kati ya hizi zinazotolewa zinakosa ubora na hazikidhi matakwa ya jamii kwa kuwa ni mbovu.

Sera ya Habari na Utangazaji Tanzania

 Ramani ya Tanzania

 Mwandishi Bishop J. Hiluka

Sera ya Habari na Utangazaji Tanzania inabainisha wazi kuwa ni haki ya msingi ya kila raia kupata au kutoa habari kama inavyotamkwa kwenye Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977. Ibara ya 18 ya Katiba inasema:
"Kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta, kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa kati. Pia kila raia anayo haki ya kupewa taarifa wakati wote kuhusu matukio mbalimbali nchini na duniani kote ambayo ni muhimu kwa maisha na shughuli za wananchi na pia juu ya masuala muhimu kwa jamii."